Mungu Mwana – Mwongozo wa Mkufunzi: Capstone Module 10 Swahili Mentor Guide

/ 1 7

M U N G U M W A N A

shauku. Kwa mtazamo wangu , jibu lake linapaza sauti kuhusu kusudi na nia ya elimu yoyote ya kweli ya Kristo katika mtazamo wa kitheolojia: “ Bwana wangu na Mungu wangu! ” Kilichoanza kwa Tomaso kama aina ya utafiti wa kiakili wenye ukaidi kuhusiana na uthibitisho wa kimwili juu ya ufufuo wa Yesu kiligeuzwa kuwa shauku iwakayo moto ya mfuasi ambaye mshangao wake unaonyesha maana halisi ya uchunguzi wa kikristolojia. “ Bwana wangu na Mungu wangu! ” Hili litakuwa ungamo la kweli, la uaminifu, na la papo hapo la kila mtu ambaye anautazama kwa umakini ukweli kuhusu Yesu wa Nazareti na, kutoka ndani ya nafsi yake, akatokea kumwona jinsi alivyo kweli kweli. Ni Roho wa Mungu pekee anayeweza kumwezesha mwanamume au mwanamke yeyote au mtoto kumwona Bwana Yesu kweli kweli; lakini, kama atafanya hivyo na kusalimisha moyo wake kwa ufunuo huo, ataungana na ukiri wa Tomaso katika maungamo binafsi ambayo yataongoza kwenye kazi, kujidhabihu, na ujasiri uleule anapotambua kwamba Mwokozi huyu mnyenyekevu lakini aliyeinuliwa, kwa kweli, ni Bwana wake na Mungu wake. Mungu na aiangazie mioyo yetu na akili zetu kupitia Maandiko, tumwone Yesu wa Nazareti jinsi alivyo hakika na tukiri pamoja na Tomaso kwa sauti kama hiyo ya shangwe na uchaji kwa mlengwa mkuu wa ibada yetu na Kiongozi wa huduma zetu: “ Bwana wangu na Mungu! ” Baada ya kutamka na/au kuimba Kanuni ya Imani ya Nikea (katika kiambatisho), sali sala ifuatayo: Mungu wa neema, Neno lako la milele alivaa mwili kati yetu pale Mariamu alipoyatoa maisha yake kulitumikia kusudi lako. Andaa mioyo yetu kwa ajili ya ujio wake tena; tufanye tuwe imara katika tumaini na waaminifu katika utumishi ili tuweze kuupokea ujio wa Ufalme wake, kwa ajili ya Kristo mtawala juu ya vyote, anayeishi na kutawala pamoja nawe na Roho Mtakatifu, Mungu mmoja, sasa na hata milele. Amina

1

Kanuni ya Imani ya Nikea na Maombi

~ Presbyterian Church (U.S.A.) and Cumberland Presbyterian Church. The Theology and Worship Ministry Unit. Book of Common Worship. Louisville, KY: Westminister/John Knox Press, 1993. p. 177.

Hakuna jaribio katika somo hili.

Jaribio

Hakuna Maandiko ya kukariri katika somo hili.

Mazoezi ya Kukariri Maandiko.

Hakuna kazi katika somo hili.

Kazi za kukusanya

Made with FlippingBook - Share PDF online