Mungu Mwana – Mwongozo wa Mkufunzi: Capstone Module 10 Swahili Mentor Guide

2 6 /

M U N G U M W A N A

Hitimisho

» Kristolojia ni elimu juu ya Yesu Kristo, maisha na kazi yake.

» Kanuni ya Imani ya Nikea inajenga uelewa wetu wa fundisho la Biblia kuhusu Yesu, kushuka kwake kutoka katika nafasi yake ya utukufu kuja duniani kwa njia ya Umwilisho ( kunyenyekezwa kwake), na kupaa kwake baada ya kifo na ufufuo wake hadi kufikia cheo cha kuinuliwa cha Bwana na Mtawala wa vyote ( kuinuliwa kwake). » Yesu ni Neno la Mungu aliyefanyika mwili, Masihi aliyetabiriwa katika Agano la Kale na kufunuliwa kwa njia ya Umwilisho wake kama Neno aliyefanyika mwili. Tafadhali chukua muda wa kutosha kujibu maswali haya na mengine yaliyoibuliwa na video. Elimu ya fundisho la Kristo ni muhimu kwa kila hatua ya maisha na huduma zetu kama wanafunzi wa Kristo. Kadiri tunavyoelewa utu na kazi yake kwa uwazi na kibiblia zaidi, ndivyo tunavyoweza kumwabudu na kumtumikia ifaavyo katika Jina lake. Maswali yaliyo hapa chini yameundwa ili kukusaidia kufanya muhtasari wa mambo muhimu yaliyofundishwa katika sehemu yetu ya kwanza. Jibu kwa usahihi na ujenge mawazo na majibu yako kwa kutumia Maandiko. 1. Nini maana ya “ Christos ” na “Kristolojia?” Kwa nini elimu ya Kristolojia ni muhimu sana kwa kila nyanja ya Imani na maisha ya Kikristo? 2. “Kashfa ya upekee” ni nini? Je, sisi kama waamini katika Kristo tunapaswa kuelewaje hoja ya upekee ya Yesu kuwa Bwana naMwokozi wa ulimwengu? 3. Je, inawezekana kwamba Mungu amejifunua mwenyewe pia kupitia dini na waokozi wengine na wakati huo huo kupitia maisha na kazi ya Yesu? Ni katika maana gani tunaweza kusema kwamba Yesu wa Nazareti ndiye njia ya mwisho na ya pekee ya kuwa na uhusiano na Mungu? Je, hii ina tafsiri gani kuhusiana na kazi ya kueneza Injili katika jamii zenye tamaduni nyingi mchanganyiko kama ya kwetu? 4. Kanuni ya Imani ya Nikea ina nafasi gani katika kutusaidia kuelewa asili ya utu na kazi ya Kristo? Je! Kanuni ya Imani inatusaidiaje kuelewa maandiko ya Biblia, yaani, yale madai ya Biblia ambayo ndio msingi wa Kanuni hiyo ya Imani? 5. Kwa nini ni muhimu kuruhusu Maandiko kuwa chanzo chenye mamlaka zaidi cha maarifa yote kuhusu Yesu Kristo? Je! tunapaswa kufanya nini

1

Sehemu ya 1

Maswali kwa wanafunzi na majibu

ukurasa 267  5

Made with FlippingBook - Share PDF online