The Kingdom of God, Swahili Student Workbook
1 0 /
UFALME WA MUNGU
Matokeo ya mwisho wa kozi yatatolewa katika mfumo wa gredi kwa kutumia skeli ya kutunuku matokeo kwa mtindo wa herufi zenye alama chanya na hasi, kisha alama za gedi yako ya ufaulu katika kazi mbali mbali zitajumlishwa na kugawanywa kwa idadi ya kazi na vipimo vingine husika ili kupata wastani wa matokeo yako ya mwisho. Kuchelewesha au kushindwa kabisa kukabidhi kazi zako kutaweza kuathiri matokeo yako. Hivyo, ni vyema kupangilia shughuli na muda wako mapema na kuwasiliana na mkufunzi wako endapo kutakuwa na changamoto yoyote. Kama sehemu ya ushiriki wako katika moduli ya Ufalme wa Mungu , utahitajika kufanya ufafanuzi (uchambuzi wa kina) wa mojawapo ya vifungu vifuatavyo vya Neno la Mungu: Mathayo 12:22-30 Marko 10:17-27 Luka 4:16-21 Luka 11:15-23 Luka 18:15-17 Isaya 11:1-9 Kusudi la kazi hii ya ufafanuzi ni kukupa fursa ya kufanya uchunguzi wa kina wa kifungu kimoja muhimu juu ya asili na kazi ya Neno la Mungu. Unaposoma mojawapo ya vifungu vilivyopo hapo juu (au andiko ambalo wewe na Mshauri wako mtakubaliana ambalo linaweza kuwa halipo kwenye orodha), imani yetu ni kwamba utaweza kuonyesha jinsi kifungu hiki kinavyoangazia au kuweka wazi umuhimu wa Neno la Mungu kwa maisha yetu ya kiroho na katika maisha yetu pamoja katika Kanisa. Pia tunatamani kwamba Roho akupe utambuzi wa jinsi unavyoweza kuhusianisha maana ya andiko hilo moja kwa moja na mwenendo wako binafsi wa ufuasi, pamoja na jukumu la uongozi ambalo Mungu amekupa kwa sasa katika kanisa na huduma yako. Hii ni kazi ya kujifunza Biblia, na ili kufanya kazi ya eksejesia , ni lazima udhamirie kuelewa maana ya andiko husika katika muktadha wake. Ukishajua andiko lilimaanisha nini kwa wasomaji wake wa kwanza, unaweza kupata kanuni zinazotuhusu sisi sote leo, na kuzihusianisha kanuni hizo na maisha. Mchakato wa hatua tatu rahisi unaweza kukuongoza katika jitihada zako binafsi za kujifunza kifungu cha Biblia: 1. Je, Mungu alikuwa akisema nini kwa watu katika muktadha wa asili wa andiko husika ? Kazi ya Ufafanuzi wa Maandiko (Eksejesia)
Dhumuni
Mpangilio na Muundo
Made with FlippingBook - Online catalogs