The Kingdom of God, Swahili Student Workbook

2 4 /

UFALME WA MUNGU

7. Uasi wa Shetani uliathiri nyanja nyingine mbili za uhai katika ulimwengu. Ni zipi, na nini kilitokea kama matokeo? 8. Tunawezaje kuelezea anguko la wanadamu – ni sababu gani tunaweza kutaja zilizopelekea uamuzi wao wa kuasi mamlaka na utawala wa Mungu Mweza wa Yote? 9. Je, jaribu la Shetani kwa Hawa linalinganaje na jinsi Yohana Mtume alivyoeleza kuhusu uovu uliomo ulimwenguni (rej. 1 Yoh. 2:16)? 10. Ni nini kilikuwa matokeo ya kusikitisha ya uasi wa Shetani huko mbinguni, na kutotii kwa Adamu na Hawa katika bustani? Wanatheolojia wanaliitaje tukio hilo baya?

1

Kupingwa kwa Utawala wa Mungu Sehemu ya 2

Mch. Dkt. Don. L. Davis

Kutotii kwa Shetani na wanadamu wawili wa kwanza kumeleta matokeo yenye kuhuzunisha na ya uharibifu katika nyanja tatu za uhai na maisha katika uumbaji: kosmos (ulimwengu), sarx (mwili wa asili ya mwanadamu), na kakos (ushawishi unaoendelea na machafuko ya yule mwovu). Kusudi letu katika sehemu hii ya pili ya somo la Kupingwa kwa Utawala wa Mungu ni kukuwezesha kuona kwamba: • Kutotii kwa Shetani na wanadamu wawili wa kwanza kumeleta matokeo yenye kuhuzunisha na yenye ya uharibifu katika nyanja tatu. • Kosmos inawakilisha muundo wa ulimwengu wa sasa na mfumo wa uasi na dhambi. • Sarx inawakilisha ubinadamu na hali ya dhambi katika asili ya mwanadamu, pamoja na kuhesabiwa hatia na matokeo ya kifo cha kimwili na kiroho. • Kakos inawakilisha kuachiliwa kwa Shetani na pepo wabaya katika nyanja ya ulimwengu na dunia, na udhibiti wake uliofuata na uendeshaji wa maisha na mifumo ya mwanadamu kupitia nguvu za uovu.

Muhtasari wa Sehemu ya 2

Made with FlippingBook - Online catalogs