The Kingdom of God, Swahili Student Workbook

3 2 /

UFALME WA MUNGU

4. Dawa ya mashitaka ya shetani: Yesu ndiye mtetezi wetu, 1 Yohana 2:1-2.

Hitimisho

» Mungu Mwenyezi ni Bwana na anatawala juu ya vyote.

» Utawala wa Mungu ulipingwa kupitia uasi wa kishetani huko mbinguni, na kupitia uasi wa hiari na kutotii kwa wanadamu wawili wa kwanza duniani. » Upinzani huo umeleta matokeo ya kusikitisha na ya uharibifu katika nyanja tatu: kosmos (ulimwengu), sarx (mwili wa asili ya mwanadamu), na kakos (ushawishi unaoendelea na machafuko ya yule mwovu).

1

Tafadhali chukua muda mwingi uwezavyo kujibu maswali haya na mengine ambayo yaliibuka kutokana na maudhui ya video. Jibu kwa uwazi na kwa ufupi, na inapowezekana, tumia Maandiko. 1. Matokeo ya kwanza ya Anguko yalikuwa ni kuibuka kwa kosmos . Neno hili la Kiyunani linarejelea nini? 2. Kosmos hufanya kazi chini ya mamlaka na udhibiti wa nani? Kuna uhusiano gani kati ya Roho Mtakatifu (ambaye hukaa ndani ya waumini) na kosmos ? 3. Kulingana na Yohana Mtume, mfumo wa sasa wa kidunia usiomcha Mungu unafanya kazi kupitia mambo gani matatu? Eleza. 4. Je, mtu anayependa kosmos ana uhusiano gani na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo? Kwa nini? 5. Sarx inawakilisha matokeo ya pili ya Anguko. Neno hili linamaanisha nini? 6. Je, ni mambo gani manne kuhusu dhambi yanayohusiana na sarx ambayo sasa yanatokea kwa watu wote kila mahali kwa sababu ya Anguko? 7. Kulingana na video, ni nini «matokeo mabaya zaidi» ya Anguko? Kakos ana nini juu ya wanadamu kuhusiana na kifo, magonjwa, na kuingilia kwake maisha na mambo ya watu wa Mungu? 8. Kulingana na Biblia, ni njia gani tatu ambazo kwazo kakos hupinga utawala wa Mungu? Je, ufahamu huu wa kakos unatusaidiaje kuelewa vyema matatizo ya majiji yetu na vita vya kiroho leo?

Sehemu ya 2

Maswali kwa Wanafunzi na Majibu

Made with FlippingBook - Online catalogs