Theology of the Church, Swahili Mentor Guide
/ 1 4 3
THEOLOJIA YA KANISA
MUUNGANIKO
Somo hili linalenga katika kufahamu asili na utendaji wa kazi ya Kanisa kupitia vigezo fulani vya Kanuni ya Imani ya Nikea, mafundisho ya Matengenezo ya Kanisa, na Kanuni ya St. Vincent. Pia tulitafuta kuelewa kazi na huduma ya Kanisa kupitia mifano au picha fulani teule zinazoangazia uhusiano wa Kanisa na kila mmoja wa washirika wa Utatu Mtakatifu, na ulimwengu, na shetani na nguvu zake za giza. Katika ulimwengu ambapo kuna wengi wanaodai kuwa Wakristo na makusanyiko yanayodai kuwa na uhusiano wa karibu sana na Mungu, ni muhimu kwamba viongozi wa Kikristo waelewe alama na vigezo vya jumuiya ya Kikristo ya kweli, na waweze kutetea na kuelezea jambo hili katikati ya wanafunzi wengine. Fikiria tena kwa uangalifu dhana hizi muhimu, na kuona jinsi zinavyotuwezesha kuelewa vizuri kazi ya Kanisa ulimwenguni. ³ Mojawapo ya vigezo muhimu zaidi na vinavyokubalika vya kuelewa asili na kazi ya Kanisa kinapatikana katika Kanuni ya Imani ya Nikea: “Tunaamini katika Kanisa moja, takatifu, katoliki na la mitume.” Kanisa la kweli ni moja, lililotengwa kuwa milki ya Mungu na kwa ajili ya matumizi yake; ni la ulimwengu wote na la kimataifa, na lina asili na utambulisho wa kitume. ³ Vigezo vya kanisa la kweli kulingana na mafundisho ya Wana-Matengenezo ya Kanisa vinakazia kanuni za Biblia, sakramenti, na taratibu za Kanisa: “Kanisa liko mahali ambapo Neno linahubiriwa ipasavyo, sakramenti zinatolewa kwa njia ipasayo, na nidhamu imepangiliwa ipasavyo.” ³ Kanuni ya Mtakatifu Vincent inalenga katika kugundua vigezo ambavyo kupitia hivyo tunaweza kupima wazo au kweli fulani ili kuona ikiwa ni yenye mamlaka ndani ya Kanisa. Kanuni hiyo inasomeka hivi: “Yale ambayo yameaminiwa kila mahali, sikuzote, na watu wote.” Kanuni hii inatoa njia ya hakika ambayo tunaweza kufuata ili kuamua kama mafundisho au mazoea fulani yanaendana na mafundisho ya “Mapokeo Makuu” ya Kanisa moja la kweli la Yesu Kristo. ³ Kwa kuelewa na kujifunza taswira mbalimbali za Kanisa katika Agano Jipya tunaweza kugundua mengi kuhusu asili na kazi ya Kanisa, utume na kazi yake ulimwenguni. ³ Kazi ya msingi ya Kanisa ni kutoa ushahidi wa kazi ya Mungu katika maisha ya kusanyiko: kazi ya kwanza ya Kanisa ni kutangaza ubora wa Mungu katika maisha na mahusiano yake. Utambulisho muhimu wa Kanisa uko katika kuwa kitu, si katika kufanya tu kitu; Kanisa, kama watu wa Mungu, limeitwa kudhihirisha ubora wa maisha unaoakisi utukufu wa Yeye aliyeliumba hapo kwanza.
Muhtasari wa Dhana Muhimu
4
Made with FlippingBook - Share PDF online