Theology of the Church, Swahili Student Workbook
/ 1 1 3
THEOLOJIA YA KANISA
MAZOEZI
Mathayo 28:18-20
Kukariri Maandiko
Ili kujiandaa kwa ajili ya darasa, tafadhali tembelea www.tumi.org/books ili kujua kazi ya kusoma ya juma lijalo, au muulize Mshauri wako.
Kazi ya Usomaji
Hakikisha umetenga muda wa kutosha kusoma kwa umakini kazi ya usomaji ijayo, na pia kutoa maoni kwa kujaza karatasi yako yenye muhtasari wa kazi za usomaji za juma husika. Pia, kufikia wakati huu katika somo lako unapaswa kuwa umechagua andiko kwa ajili ya kazi yako ya ufafanuzi, na uwe umetoa pendekezo lako kuhusiana na kazi ya huduma kwa vitendo. Ikiwa hujafanya hivyo, tafadhali fanya hivyo haraka iwezekanavyo. Somo letu linalofuata linahusiana moja kwa moja na mada ya somo la tatu. Somo letu linalofuata linaitwa, «Kanisa katika Kazi,» na lengo lake ni kuelewa vipengele mbalimbali vya Kanisa, na jinsi tunavyoweza kugundua jumuiya ya Kikristo ya kweli kupitia matendo na mtindo wa maisha wa Kanisa. Tutatumia alama na ufafanuzi unaotokana na Kanuni ya Imani ya Nikea, mafundisho ya Matengenezo ya Kanisa, na kanuni ya Mtakatifu Vincent ili kuelewa na kutathmini tofauti kati ya makusanyiko ya kweli na yasiyo ya kweli. Pia tutaangalia kazi za Kanisa kupitia picha mbalimbali ambazo tutazitumia kama msingi wa kuelewa kile ambacho Kanisa linapaswa kufanya katika maisha na utume wake. Picha hizi zitajumuisha nyumba ya Mungu, mwili wa Kristo, na hekalu la Roho Mtakatifu, mabalozi wa Kristo, na jeshi la Mungu.
Kazi Zingine
Kuelekea Somo Linalofuata
3
Made with FlippingBook flipbook maker