Theology of the Church, Swahili Student Workbook

8 /

THEOLOJIA YA KANISA

Muhtasari wa Mfumo wa Kutunuku Matokeo na Uzito wa Gredi

Mahitajai ya Kozi

Mahudhurio na Ushiriki Darasani

30% alama 90 10% alama 30 15% alama 45 15% alama 45 10% alama 30 10% alama 30

Majaribio

Kukariri Maandiko

Kazi ya Ufafanuzi wa Maandiko

Kazi ya Huduma

Kazi za Usomaji na za Kufanyia Nyumbani

Mtihani wa Mwisho

10% alama 30 Jumla: 100% alama 300

Mambo ya Kuzingatia katika Utoaji Maksi

Kuhudhuria kila kipindi ni moja ya masharti ya msingi ya kozi hizi. Kukosa kipindi kutaathiri matokeo yako. Ikiwa una dharura isiyoepukika itakayokulazimu kukosa kipindi, tafadhali mjulishe mkufunzi wako mapema. Ukikosa kipindi ni jukumu lako kutafuta taarifa kuhusu kazi na mazoezi yaliyotolewa, na kuongea na mkufunzi wako pale inapobidi kufanya na kukabidhi kazi kwa kuchelewa. Sehemu kubwa ya mafunzo yanayohusiana na kozi hii hufanyika kupitia mijadala. Kwa sababu hiyo, unahimizwa na kutarajiwa kushiriki kikamilifu katika kila kipindi cha kozi hii. Kila kipindi kitaanza na jaribio fupi kuhusu mawazo ya msingi yaliyofundishwa katika somo lililopita. Njia nzuri zaidi ya kujiandaa na majaribio haya ni kupitia Kitabu cha Mwanafunzi na daftari uliloandikia maelezo ya somo hilo lililopita. Kukariri Neno la Mungu ni kipaumbele cha msingi kwa maisha na huduma yako kama mwamini na kiongozi katika Kanisa la Yesu Kristo. Kozi hii ina mistari ya Biblia michache, lakini yenye umuhimu mkubwa katika jumbe zake. Katika kila kipindi utahitajika kukariri na kunukuu (kwa mdomo au kuandika) mistari ya Biblia uliyopewa na mkufunzi wako. Neno la Mungu ni zana yenye nguvu ambayo Mungu anaitumia ili kuwaandaa watumishi wake kwa kila kazi ya huduma aliyowaitia (2 Tim. 3:16-17). Ili kutimiza matakwa ya kozi hii, lazima uchague kifungu cha Biblia na kufanya uchambuzi wa kina (yaani, eksejesia au ufafanuzi wa Maandiko). Kazi yako iwe na kurasa tano (ziliyochapwa kwa kuacha nafasi mbili kati ya mistari au kuandikwa vizuri kwa mkono), na kushughulikia mojawapo ya vipengele vinne vya Kanisa vinavyozungumziwa katika masomo manne ya kozi hii. Ni shauku na matumaini yetu kwamba utashawishika kikamilifu na kuamini juu ya uwezo wa Maandiko kuleta badiliko na athari chanya katika maisha yako na ya wale unaowahudumia.

Mahudhurio na Ushiriki Darasani

Majaribio

Kukariri Maandiko

Kazi za Ufafanuzi wa Maandiko

Made with FlippingBook flipbook maker