https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 1 5

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

na huduma yako ndani ya kanisa lako na kupitia kanisa lako. Kwa hivyo, sehemu hii muhimu ya kukamilisha moduli hii itakuhitaji kubuni kazi ya huduma kwa vitendo ili kukusaidia kushirikisha wengine baadhi ya maarifa ambayo umejifunza katika kozi hii. Andiko la 1 Petro 2:9-10 linalielezea Kanisa kama taifa, ukuhani, na watu. Hakuna neno lolote kati ya haya linaloturuhusu kuuelewa wokovu wetu kama suala la mtu binafsi lisilohusiana na kusanyiko. Lengo la kazi hii ya huduma kwa vitendo ni kukusaidia kuimarisha ujuzi wako katika kuelezea uhusiano kati ya wokovu na Kanisa. Tafadhali kamilisha kila moja ya hatua zifuatazo: Tambua na uelezee kwa ufupi kwa maandishi hali fulani katika uzoefu wako wa zamani au wa sasa ambapo mtu unayemjua anadai kwamba hafikirii Kanisa kuwa ni sehemu muhimu ya maisha yake ya kiroho. (Unaweza kutumia jina la kubuni kwa ajili ya mtu huyu ikiwa ungependelea kuficha utambulisho wake). Namna hii ya kuliupuuzia Kanisa inajidhihirisha katika maneno yake; “Sijisikii kama ni lazima niende kanisani ili kumwabudu Mungu!” Au inaweza kujionyesha katika tabia yake; anadai kuwa ni Mkristo mzuri lakini mahudhurio yake kanisani ni ya mara chache sana. Andika mfano wa barua kwa mtu huyu ukianisha kwa maneno yako mwenyewe sababu ambazo zinakufanya uamini kwamba ameelewa vibaya kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu wokovu na Kanisa. Maudhui ya barua hiyo yanapaswa kutokana na theolojia ambayo umejifunza katika kozi hii, na yaonyeshe ufahamu wako wa theolojia hiyo. Lengo la barua hii ni kuhamishia mawazo na dhana za kitheolojia katika uzoefu wa kivitendo. Hili si “andiko la kitheolojia,” bali ni wasilisho la mafundisho ya kibiblia ya kweli kwa mtu ambaye anaonyesha kuwa na uelewa potofu wa Maandiko au ameamua kwa makusudi kuyaasi Maandiko. Kabidhi nakala ya barua kwa mwalimu wako. Kisha, tafakari katika maombi ikiwa Mungu anaweza kukuruhusu umfikie mtu uliyeandika habari zake (ikiwa ni jambo lililopo sasa) na umtumie barua hiyo au kuzungumza naye ana kwa ana kuhusu wokovu wake na maisha ya kanisa. Kazi ya huduma inabeba alama 30 ambazo zinawakilisha 10% ya jumla ya maksi zako, hivyo hakikisha unashirikisha yale uliyojifunza kwa ujarisi na ripoti yako iwe yenye kueleweka vizuri.

Mpangilio na Muundo

Hatua ya Kwanza

Hatua ya Pili

Hatua ya Tatu

Utoaji maksi

Made with FlippingBook Annual report maker