https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi

/ 2 6 5

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

Orodha Hakiki ya Vipengele vya Simuli (muendelezo)

VIII. Kwa Namna gani Wahusika wana Ongezeka na Kukua (au kupungua na kuanguka) katika Hadithi? A. Ni wapi wahusika wanaanzia katika hadithi? B. Ni kwa namna gani yale wanayokutana nayo wahusika yana athiri kuendelea kwao? C. Ni sehemu gani ambapo wahusika mmoja mmoja wanafikia mwisho kama matokeo ya yale waliyokuwa wanayapitia, na maamuzi waliyoyafanya baina yao? IX. Ni Ushindani, Kejeli na Haki zipi Zilizotumika katika Hadithi? A. Ushindani: Ni wahusika gani wamewekwa ili kuwa kama washindani katika hadithi hii? B. Kejeli: Ni wakati gani msomaji anataarifiwa kuhusiana na hali na uhalisia ambao wahusika wenyewe hawafahamu? X. Ni Vipengele Gani Vimerudiwa, Vimesisitizwa, na Vimepewa Umuhimu Zaidi katika Hadithi? A. Marudio: Ni kauli gani, vipengele gani, dhamira, masuala na matendo ambayo yanajirudia? B. Msisitizo : Vitu gani katika wahusika na matukio ambayo yamesisitiziwa zaidi kuliko vitu vingine? C. Kupewa umuhimu zaidi: Vitu gani vimepewa umuhimu zaidi kama “msingi” Katika mwendelezo wa hadithi? XI. Ni nini Msimamo wa Mwandishi wa Hadithi ? A. Ni maoni gani mwandishi anatupa kuhusu wahusika na matukio katika hadithi? B. Ni hisia gani unaamini hadithi inalenga kuzalisha? C. Ni kwa jinsi gani vitu na taarifa zimepangwa ili kuwasilisha msimamo wa mwandishi kwa ufasaha?

Made with FlippingBook Annual report maker