https://user-fNLORqa.cld.bz/Misingi-ya-Utume-wa-Kikristo-Mwongozo-wa-Mkufunzi
3 0 2 /
MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO
Ili Tuwe Umoja (muendelezo)
2. Liturujia na sherehe zinazofanana (yaani, ibada inayofanana ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa maskini wa mijini zinapaswa kuakisi msingi mmoja wa utunzi na uimbaji wa nyimbo, uendeshaji wa sakramenti, mwelekeo na taswira ya kitheolojia, mtazamo kuhusu ujumi, mavazi, utaratibu wa kiliturujia, ishara, na malezi ya kiroho ambayo yanatuwezesha kumwabudu na kumtukuza Mungu kwa njia inayomwinua Bwana na kuwavuta watu wa mijini kwenye ibada yenye uhai. 3. Ushirika mmoja, afya, ustawi, na ufadhili wa pamoja (yaani, utaratibu mmoja na msingi mmoja wa nidhamu ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa maskini wa mijini lazima zijengwe katika mahubiri halisi ya Injili ya kiinjili na ya kihistoria ambayo yanasababisha watu wampokee Yesu Kristo kama Bwana na kuingizwa katika makanisa ya mahali. 4. Katekisimu na mafundisho ya pamoja (yaani, imani moja ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa maskini wa mijini lazima zikumbatie theolojia moja ya kibiblia na kuiakisi kwa vitendo elimu ya Kikristo inayoakisi imani yao ya pamoja. 5. Mfumo Mmoja wa Utawala na Mamlaka ya Kanisa (yaani, sera ya pamoja ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa maskini wa mijini lazima ziratibiwe kulingana na sera ya pamoja, mfumo mmoja wa usimamizi wa kanisa, na kujitiisha kwa sera nyumbufu za uongozi zinazoruhusu usimamizi mzuri na wenye ufanisi wa rasilimali na makusanyiko yao. 6. Mfumo wa pamoja wa maendeleo ya uongozi (yaani, mkakati wa pamoja wa uchungaji ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa maskini wa mijini zinajizatiti kuhakikisha kila kusanyiko lina wachungaji wanaomcha Mungu, na zinatafuta kutambua, kuandaa, na kuunga mkono wachungaji na wamishenari wake ili washirika wao wakue hata kufikia ukomavu katika Kristo. 7. Falsafa na utaratibu wa kifedha wa pamoja (yaani, msingi mmoja wa uwakili ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa watu maskini wa mijini zinajitahidi kushughulikia masuala yao yote ya kifedha na rasilimali kwa kutumia sera zenye hekima, zilizoboreshwa, na ambazo kila kusanyiko linaweza kuzitumia, zinazoruhusu usimamizi mzuri wa fedha na rasilimali zao, ndani, kikanda, na kitaifa. 8. Huduma ya pamoja ya utunzaji na uwezeshaji (yaani, msingi mmoja wa huduma ). Harakati za Kupanda Makanisa miongoni mwa maskini wa mijini
Made with FlippingBook Annual report maker