Kutafsiri Biblia: Capstone Module 5 Swahili Student Workbook
/ 2 1 9
K U T A F S I R I B I B L I A
wa Biblia na madai ya usomi wa kisasa wa Biblia, na kuona jinsi Neno la Mungu lilivyovuviwa na Mungu, kwa maana waandishi waliongozwa na Roho Mtakatifu na hivyo maandiko waliyoandika ni maneno yaliyovuviwa na Mungu Aliye Hai. Mbinu ya Hatua Tatu imetupatia kielelezo chenye ufanisi ili kuelewa maana ya Biblia katika muktadha wake yenyewe, kupata kanuni za kibiblia na kutumia maana yake kwa njia za vitendo katika maisha yetu chini ya maelekezo na uongozi wa Roho. Mbali na maarifa haya, pia tumefafanua umuhimu wa elimu ya tanzu katika kutafsiri Biblia, na kuangalia umuhimu wa masimulizi na unabii katika kutafsiri Biblia. Hatimaye, tulichunguza safu ya zana, za msingi na za ziada, zilizoundwa ili kutusaidia kuunganisha umbali kati ya uelewa wetu wa matini ya kale na matumizi yetu wenyewe ya Neno la Mungu leo. Bila kujali ni njia gani au zana gani tunazotumia, hakuna kitu kinachoweza kufanyika mbadala wa jitihada zetu binafsi za kujifunza Neno la Mungu kwa nidhamu, sala, na utii. Pasipo usaidizi na uongozi wa Roho, hatuwezi kuelewa maana ya maandiko. Hata hivyo, ikiwa sisi ni wanyenyekevu na wenye bidii, kweli ya Neno itakuja maishani mwetu na kutubadilisha tunapo mtumikia Bwana wetu tukiwa wanafunzi wa Ufalme. Sio tu kwamba kujifunza namna hiyo kutatubadilisha, bali pia Mungu atatutumia kama vyombo vya kuwasilisha Neno lake katika Kanisa na ulimwengu, yote kwa utukufu wake. Mungu na atupe shauku na nguvu ya kuwa watenda kazi wanaojifunza ili kujithibitisha wenyewe kuwa ni watenda kazi wenye bidii katika Neno la Mungu, tukilitumia kwa halali Neno lake kamilifu na la kweli, ili tumjue Kristo na kumfanya ajulikane, yote kwa ajili ya utukufu wake mkuu zaidi. Amina na amina!
4
Made with FlippingBook Digital Proposal Maker