Misingi ya Utume wa Kikristo, Mwongozo wa Mkufunzi

/ 2 1 9

MISINGI YA UTUME WA KIKRISTO

kwa maskini, kwa msingi wa ukombozi wa Mungu kwao katika “Kutoka”, na walipaswa kuonyesha shalom ya Bwana katika mahusiano yao yote na kushughulika kwao na watu wengine. ³ Yesu ndiye mwanzilishi na Kichwa cha Kanisa, Jamii ya Ufalme wa Mungu ya Agano Jipya, ambayo imeitwa kuonyesha shalom ya Mungu katikati ya watu wa Mungu leo. ³ Yesu alijitambulisha kama Masihi yule wa unabii na ahadi ya A.K. Alianzisha huduma yake ya Kimasihi kwa matendo ya kuponya walioonewa na kuhubiri habari njema kwa maskini. Alithibitisha umasihi wake kwa Yohana Mbatizaji kupitia matendo ya haki na kuwahubiria maskini. Alihakiki na kuthibitisha wokovu wa watu kwa kwa kuzingatia namna walivyowatendea maskini, na alijihusisha kikamilifu na “walio wadogo” (yaani, wenye njaa, wenye kiu, wageni, walio uchi, wagonjwa, na wafungwa). ³ Kanisa ni jamii ya ufalme wa Mungu. Limeitwa kutangaza Habari Njema ya Ufalme kwa maskini, kutendeana kama mwili wa Kristo kila mmoja kwa mwingine, na kutoa ushahidi wa maisha ya Enzi Ijayo kwa kuonyesha kielelezo cha utendaji wa haki katika ulimwengu. Kupitia maisha na utume wa Kanisa, kwa uweza wa Roho Mtakatifu, Watu wa Mungu leo wanaonyesha na kufurahia shalom ile ile inayozungumzwa katika Agano la Kale. ³ Kanisa linaitwa kuonyesha ukarimu wa hali ya juu kwa wahitaji, kwa kuwapa kipaumbele cha pekee wale walio ndani ya jamii ya waaminio, hasa wajane, yatima na maskini. Pia tunawajibu wa kutoa misaada kwa makanisa mengine wakati wa misiba na dhiki. ³ Kama mwili wa Kristo ulimwenguni, Kanisa limeitwa kuwa mtetezi wa maskini, ambayo ni alama ya utume halisi wa Kikristo. Utetezi huu unajumuisha kutenda haki (yaani, kutokuwa na ubaguzi wala upendeleo kwa sababu ya tabaka au utofauti) katika mwili, kutenda matendo mema kwa niaba ya maskini na walio hatarini, na kufanya kazi ili kusaidia kukidhi mahitaji halisi ya wengine, hasa wale walio katika nyumba ya Mungu. ³ Kuhusu utume wa mijini, Kanisa limeitwa kutangaza Habari Njema kwa maskini, hilo ni pamoja na kuwaheshimu kama walivyochaguliwa na Mungu na kama watu ambao Kristo alijitambulisha nao. Hatupaswi kamwe kuwadhalilisha, bali kushughulika nao kwa haki na huruma, tukiwa na uhakika kwamba wanaweza kugeuzwa na kuchangia katika maendeleo ya Ufalme.

4

Made with FlippingBook - Online catalogs