Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi

124 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I

Wakristo wengine, na viongozi wetu inahitaji uwazi na hekima. Wanazuoni, wafanyakazi wa kanisa, wachungaji na wahubiri, na walei (wasio na wadhifa katika Kanisa) kwa pamoja wametatizika na maswali yahusianayo na ufasiri wa Biblia kwa karne nyingi, na sasa ni nafasi yako ya kujiunga na mjadala huu! Tumia maswali yaliyo hapa chini ili kuanzisha safari yako ya kiutafiti kuhusu asili ya jitihada zako mwenyewe za kujifunza Biblia. • Pamoja na kuchanganyikiwa na mashaka yote yanayosababishwa na uhakiki wa kisasa wa Biblia, je, tunapaswa kuwa na mashaka katika kutumia njia yoyote, ikiwa ni pamoja na Mbinu ya Hatua Tatu kama mbinu tuliyoichagua ya kujifunza maandiko? Je, tunajuaje kwamba hata Mbinu ya Hatua Tatu haitapindishwa na kusababisha kukanushwa kwa mafundisho halisi ya imani ya Kikristo? • Tunawezaje kuwa na uhakika kwamba kutumia mbinu kama Mbinu ya Hatua Tatu si namna tu iliyoboreshwa ya kukinzana iwezayo kufikirika na kutajwa chini ya jua, tunahakikishaje kwamba mafunuo yote tunayoyapata katika kujifunza kwetu yanakubaliana na ujumbe wa Biblia nzima? Je, tunaepukaje kujikita katika mambo yasiyo ya msingi katika kujifunza kwetu Biblia? Toa mifano halisi. • Je, viongozi wetu (yaani, maaskofu, wachungaji, washauri, viongozi wa Kikristo wanaotambulika, n.k.) wana jukumu gani katika kuchukulia tafsiri zetu binafsi kama mafundisho yenye mamlaka ya Neno? Je, tunapaswa kushikilia tafsiri ya maandiko ambayo tumeipata katika kujifunza kwetu endapo inakinzana na yale ambayo Ukristo umefundisha katika kanuni za imani na katika historia nzima ya Kanisa? Elezea. • Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuwaruhusu wengine kuhakiki na kukosoa matokeo ya kujifunza kwetu na mawazo yetu kabla hatujatangaza kwamba tumegundua kanuni za jumla ambazo zinawahusu wakristo wote? Je, ni mitazamo ya aina gani tunapaswa kuonyesha tunapozungumza kuhusu mambo mapya ambayo tumejifunza kutoka kwa Bwana? • Je, tunapaswa kumchukuliaje mtu, hata awe mwanazuoni na msomi mbobevu, ambaye hataki mawazo yake kupimwa na kukaguliwa kwa mujibu wa mafundisho ya Biblia yenyewe? Je, ni kwa jinsi gani mfano wa Waberoya na mwitikio wao kuhusiana na mafundisho ya Paulo unatukumbusha jukumu letu la kuwa tayari kuchunguza tafiti za wengine kwa kuzilinganisha na maandiko yenyewe (rej. Mdo. 17:11)? na “usitegemee akili zako mwenyewe” (Mit. 3:5-6)? • Kwa wingi wa tafiti zinazofanyika kuhusu kila mada

2

M A S O M O Y A B I B L I A

Made with FlippingBook Digital Proposal Maker