Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi
126 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I
Tunawezaje Kuthibitisha kitu Chochote kutoka katika Maandiko Matakatifu? (Inatokana na kisa cha kweli). Akiwa katika Chuo akichukua Shahada ya Uzamili, mchungaji chipukizi alikumbana na wazo ambalo lilimpa changamoto na kumchanganya kwa kiasi fulani. Wakati wa somo kuhusu mbinu za uchunguzi wa kisayansi wa dini, aliambiwa na profesa wa somo hilo kwamba kutumia tu Biblia kuthibitisha hoja za Biblia ni “tautolojia,” au kutengeneza mzunguko wa ubishi usioweza kuthibitisha chochote. Profesa huyo aliendelea kusema: “Ikiwa unataka kuthibitisha kwamba jambo fulani katika Biblia ni la kweli, huwezi kutumia Biblia hiyo hiyo kulithibitisha. Katika mbinu ya kisayansi unathibitisha mambo kwa msingi wa uthibitisho wa kujitegemea , si kwa msingi wa wale ambao wana faida binafsi kutokana na matokeo ya utafiti.” Profesa huyo aliendelea kudokeza kwamba kwa sababu manabii na mitume walimwamini Kristo, walikuwa katika hatari kubwa endapo wangesema jambo lolote kinyume na Yesu isipokuwa yale ambayo walitaka watu wengine waamini. Kwa sababu hiyo, alisisitiza, hatuwezi kuchukua ushuhuda wao kuhusu Yesu wa Nazareti na madai yake kuwa wa kweli. Akiwa amechanganyikiwa, mchungaji huyu darasani alijihisi kama mtu aliyevunjwa miguu kabisa. Anawezaje kuthibitisha fundisho la maandiko bila kutumia maandiko yenyewe kama ushahidi? Unafikiri nini kuhusu maoni ya profesa, na ungemshauri mchungaji afanye nini ili aweze kukamilisha masomo yake katika kozi ile? Biblia yako Katika Lugha ya Asili Haitoshi! (Inatokana na kisa cha kweli). Alipokuwa akikusanya kazi yake ya ufafanuzi (exegetical project) katika somo la kitabu cha Warumi, mwanafunzi mmoja aliambiwa na profesa wake (ambaye alikuwa amesahihisha kazi yake ya kwanza ya somo hilo) kwamba alikuwa amevunja kanuni za msingi katika kutumia zana za lugha. Profesa huyo alieleza hivi: “Huwezi kwenda kwenye kamusi ya kitheolojia au kamusi ya lugha na kudhania kwamba matumizi yote ya neno fulani yaliyoandikwa humo ndizo maana zilizokusudiwa mahali hapa . Hungetumia kamusi ya Kiingereza au Kihispania kwa njia hiyo; ungetafuta neno, ukapata ufafanuzi unaofaa katika muktadha wa kazi yako, na kisha utumie maana hiyo moja . Wewe umetumia maana zote za neno katika uandishi wako, na kwa sababu hiyo ukafanya makosa makubwa katika kazi yako.” Profesa huyo aliendelea kusema kwamba ni pale tu unapojua jinsi mwandishi mmoja-mmoja alivyotumia neno (kwa mfano, namna neno fulani lilivyotumiwa na Petro, Paulo, au Yohana katika uandishi wake wote) ndipo unaweza kuwa na uhakika kwamba unatumia vyanzo vyako vya lugha ipasavyo. Kwa kuwa Biblia iliandikwa katika Kiebrania, Kiaramu, na Kiyunani, na kwa kuwa wengi wetu hatujui lugha hizi, tunawezaje
2
2
M A S O M O Y A B I B L I A
3
Made with FlippingBook Digital Proposal Maker