Mtaala wa Cornerstone, Kitabu cha Mwanafunzi
62 / MTAALA WA CORNERS TONE K I TABU CHA MWANAFUNZ I
nzuri katika muongo uliopita wa mada za haki. Upande hasi wa kuishi katika enzi ya “tenda wema” ni kwamba mara nyingi Wakristo hawaunganishi kazi zao za utetezi wa haki na maisha yao ya kiroho. Kama kampuni ya Nike, wanafanya tu. Tunapofanya matendo mema, isiwe tu kwa ajili ya kutenda. Ikiwa tunapaswa kuchukua Waefeso 2:10 kwa uzito, ni kwamba tuliumbwa kuyatenda. Fikiria hilo kwa dakika moja. Hatujaokoka ili tu kukaa tu na kuwa na mafunzo ya Biblia tukisherehekea jinsi tulivyo watakatifu. Yakobo 2:14-26 inaweka wazi kabisa hakuna namna tunaweza kutofautisha au kutenganisha imani na matendo. Kwa kweli huwezi kuwa na kimojawapo bila kingine. Ikiwa ni hivyo, kazi yetu ya kupambana na umaskini inapaswa kuwa msingi wa imani yetu kwa njia ya vitendo. Kihistoria, kumekuwa na jumuiya za kidini ambazo zimejitolea kwa ajili ya utume na kuunda kanuni za maisha ili kuwasaidia kuendeleza utume huo. Ni mfumo wa utendaji ambao umestahimili mtihani wa wakati. Matumizi ya kanuni za maisha yanaweza kupatikana katika Biblia. Tunaona hili katika kitabu cha Danieli, ambapo yeye na wenzake walijiwekea miiko ya namna kubaki kuwa waaminifu wakiwa uhamishoni BHabili (Dan. 1; 6:10). Pale ambapo kanuni ya maisha inafanya kazi vizuri, ni kielelezo cha maisha ya kujitoa kikamilifu. Ni onyesho la vitendo la jinsi ya kumfanya Mungu kuwa kitovu cha utume na utumishi wetu, akitusogeza katika utakatifu.
Tamka na/au imba Kanuni ya Imani ya Nikea (katika kiambatisho).
Kanuni ya Imani ya Nikea
4
K A Z I Y A K I U K O M B O Z I D H I D I Y A U M A S K I N I
Kariri Yohana 1:14 kwa kutumia Biblia ya kawaida (si toleo lililofafanuliwa), kisha ujisahihishe mwenyewe kwa kutumia Fomu ya Kusahihisha Ukariri wa Maandiko.
Kukariri Maandiko
Ili kujiandaa kwa ajili ya darasa, rejelea ratiba ya kozi hii ili kuona kazi zinazopaswa kufanyika kabla ya mkutano wako ujao wa darasa na ukamilishe kazi zilizo hapa chini: Soma yafuatayo: • Kazi ya Kiukombozi dhidi ya Umaskini – “Mienendo ya Maisha na Kazi ya Umaskini” (uk. 37-50) • Kania Lisilo la Kawaida: Mabadiliko ya Jamii kwa Manufaa ya Wote – Sura ya 1: Utetezi Pekee Hautoshi
Kazi
Made with FlippingBook Digital Proposal Maker