Mtaala wa Cornerstone, Mwongozo wa Mkufunzi
M W O N G O Z O WA M K U F U N Z I / 2 7
A. Kanuni za Uwezeshaji za Agano la Kale Wasaidie wanafunzi wako kuelewa yafuayo: 1. Agano la Kale lilijikita katika kutengeneza njia za fursa. 2. Biblia si lazima izingatie sababu. Agano la Kale lililenga katika kutengeneza njia za fursa kwa watu kuweza kustahimili hali zao au kuvuka hali zao na kuelewa kwamba Mungu ni mkuu kuliko hali wanazojikuta ndani yake. • Mfano wa hili ni kanisa ambalo lilitoa ufadhili kamili wa masomo kwa watoto wampendao Mungu walio katika umaskini, ambao walikuwa na uwezo na shauku ya kwenda chuo kikuu, lakini sio fursa. Kwa kupata shahada ya chuo kikuu, wamekuwa wanajamii wenye tija na hawako tena katika umaskini. 3. Tungeweza hata kusema kwamba muktadha wa Biblia katika ujumla wake ni wa hali ya umaskini kwa sababu karibu katika kila utamaduni, unadharauliwa ikiwa hauna rasilimali za kutosha (raia wa daraja la pili). • Katika Biblia, taifa la Israeli halikuonekana kama taifa lenye nguvu, bali kama kundi la watu wakorofi waliokuwa utumwani. Hata hivyo, Mungu alisema wao, watu wa chini, wangekuwa watu wake. Msingi mzima wa kitabu cha Kutoka ni kwamba Mungu aliwatoa Misri.
4 Ukurasa wa 34 Muhtasari wa Kipengele A
1
K A Z I Y A K I U K O M B O Z I D H I D I Y A U M A S K I N I
• Pia, kulikuwa na watu/mataifa mengine huko Misri, na walipoona kile Mungu wa Waisraeli alichofanya,
walikwenda pamoja na wana wa Israeli. Waliona kile Mungu alichofanya kwa taifa “lenye nguvu” la Misri na jinsi Mungu alivyomnyenyekeza mungu wa Misri.
B. Yesu Alipendelea Maskini / C. Yesu Alionya dhidi ya Utajiri Angazia yafuatayo kuhusu vipengele hivi viwili vya muhtasari: 1. Yesu na wahusika wengi wa Biblia walikuwa maskini wafanyao kazi.
5 Ukurasa wa 35 Muhtasari wa Kipengele B na C
Made with FlippingBook - professional solution for displaying marketing and sales documents online