Mtaala wa Cornerstone, Mwongozo wa Mkufunzi

2 8 / M T A A L A WA C O R N E R S T O N E M W O N G O Z O WA M K U F U N Z I

2. Yesu alichagua kuishi katika hali duni ya kufanya kazi. 3. Yesu alikuwa anaweka mkazo mkubwa sana kwa kuonyesha kwa vitendo kwamba tunahitaji kuwathamini watu walio katika umaskini. 4. Yesu alichagua kuwa rabi ambaye hakuwa na heshima nyingi na mamlaka nyingi za kidunia. Alifanya hivyo akiweka kielelezo cha unyenyekevu. 5. Mungu anaweza kuvuka mipaka ya popote ulipo kama mtu, au kama kanisa, kama ilivyo katika Kitabu cha Matendo. 6. Uwezeshaji ni muhimu zaidi kuliko sababu. • Lenga katika kuunda njia za fursa. • Kwa watu wanaoishi katika hali ya umaskini, wajue huo si utambulisho wao, bali ni hali wanayoishi. • Tunapaswa kuheshimu talanta na uwezo wao na kuelewa kwamba Mungu atazitumia. Sasa waruhusu wanafunzi watoe maoni yao juu ya kile kilichowasilishwa. Hapa kuna baadhi ya mada ambazo zinaweza kujadiliwa ikiwa unahitaji kuendeleza mjadala. (KUMBUKA: Haulazimiki kuzitumia. Ikiwa darasa lako linakwenda vizuri, waruhusu wanafunzi wajadili kwa uhuru). • World Impact hutoa mafunzo ya ngazi ya seminari yenye ufanisi, nafuu, na rahisi kuyapata, jambo ambalo ni njia ya fursa. Hili linatokana moja kwa moja na Maandiko. • Sababu kuu inayosababisha wachungaji wasipate mafunzo rasmi ni ukosefu wa pesa. • Shirika lisilo la kiimani linaweza kuchukua baadhi ya kanuni za Kazi ya Kiukombozi dhidi ya Umaskini na kufanya mambo mazuri; wanaweza kuifanya dunia kuwa mahali pazuri zaidi. Sehemu ya Kazi ya Kiukombozi dhidi ya Umaskini ni Kazi ya Kupambana na Umaskini kwa misingi ya kimaadili.

1

K A Z I Y A K I U K O M B O Z I D H I D I Y A U M A S K I N I

 6 Ukurasa wa 37 Maswali kwa Mwanafunzi na Majibu

Made with FlippingBook - professional solution for displaying marketing and sales documents online