Mtaala wa Cornerstone, Mwongozo wa Mkufunzi
M W O N G O Z O WA M K U F U N Z I / 2 9
• Jadili kuhusu wafanya kazi maskini katika huduma. Mungu amemuumba kila mmoja wetu kwa kusudi na ametupa karama na talanta ili tuweze kutoka na kuifanya dunia kuwa mahali pazuri zaidi. Kwa hivyo, ikiwa tutatoka na kujaribu kufanya yale tuliyoumbwa kufanya na kueneza Ufalme, kutakuwa na upaji wa kutosha kukidhi mahitaji yetu. • Mwanzo 3 inaweka wazi kabisa kwamba tunaishi katika ulimwengu ulioanguka, kwa hiyo tutegemee kukutana na magumu katika maisha yetu. Mungu atatumia magumu hayo tunaposhughulika na wengine. Mungu atageuza mitihani yetu kuwa ushuhuda. Amini katika ahadi za Mungu kwamba hatimaye, kila kitu kitakuwa sawa ingawa unaweza usione hayo katika wakati wa maisha YAKO. • Walio wengi hawafanikiwi kuondokana na umaskini. • Sababu kubwa kwa nini watu wako katika umaskini ni kwamba walizaliwa humo. • Au tumia yafuatayo kwa ajili ya majadiliano darasani: 1. Kwa nini watu hawana ufahamu wa Kibiblia 2. Mbali na kuwa kipaumbele cha ufalme, ni sababu zipi tatu kuu za kujihusisha na Kazi ya Kupambana na Umaskini katika mtazamo wa kibiblia? 3. Je, kuna sababu halali za kutojihusisha nayo? Jadili Mfano Halisi Mtumishi kijana wa mjini ambaye anasimamia watu wanaojitolea kutoa mafunzo kwa ajili ya programu ya kufundisha shule katika mtaa maskini amekuja kuomba ushauri. Kazi yake ni kutoa semina elekezi kabla ya wanaojitolea kupewa watoto wa kufanya nao kazi. Amegundua kuwa mara kwa mara anaingia kwenye shida. Kila semina elekezi mjadala unazuka miongoni mwa watu wapya wanaojitolea kuhusu sababu za umaskini. Kundi moja linasema kwamba watu ni maskini kwa sababu walifanya maamuzi mabaya katika maisha yao. Wengine wanadai kuwa watu ni maskini kwa
1
K A Z I Y A K I U K O M B O Z I D H I D I Y A U M A S K I N I
7 Ukurasa wa 38 Mfano Halisi
Made with FlippingBook - professional solution for displaying marketing and sales documents online