Mtaala wa Cornerstone, Mwongozo wa Mkufunzi

4 0 / M T A A L A WA C O R N E R S T O N E M W O N G O Z O WA M K U F U N Z I

II. Kazi ya Kiukombozi katika Biblia Sifa za Kazi ya Kiukombozi dhidi ya Umaskini: • Uwezeshaji wa kimaadili.

 3 Ukurasa wa 55 Muhtasari wa Kipengele cha II

• Urejesho bora kupitia dhabihu. • Mungu ni mkuu kuliko mazingira. • Umaskini ni hali, si utambulisho. • Enenda kwa imani huku ukipanga upya nguvu za kimfumo za binadamu. 1. Uwezeshaji wa kimaadili • Ninajidhabihu, unashinda. Namna tunavyofanya kazi zi muhimu. Mwitikio wa watu ni wa muhimu na wa kuzingatiwa sana. • Haihusiani na sisi tu, haihusiani na wao tu, ni kuhusu kufanya kazi pamoja kwa ushirikiano ili Mungu aweze kupokea utukufu wote. 2. Urejesho bora kupitia dhabihu • Kielelezo ambacho Kristo alitumia kutukomboa. • Kwa sababu ya yale ambayo Yesu ametufanyia, tunataka kufanya hivyo kwa ajili ya wengine. • Unafanya hivi na unajaribu kufanya kazi ili kufanya hali kuwa bora kwa watu wanaoishi katika hali ya umaskini, kwamba inakunufaisha au la. Utajitolea na kujaribu kufanya maisha yao kuwa bora, kama vile Kristo alivyofanya kwa ulimwengu mzima. 3. Mungu ni mkubwa kuliko mazingira. • Hii ni dhahiri lakini inasahaulika kwa urahisi. • Mungu ni mkubwa kuliko mazingira tunayoyaona, na Mungu ni mkubwa licha ya mazingira.

3

K A Z I Y A K I U K O M B O Z I D H I D I Y A U M A S K I N I

Made with FlippingBook - professional solution for displaying marketing and sales documents online