Mungu Baba: Swahili Module 6 Mentor Guide

/ 2 7 3

M U N G U B A B A

Mifano ya rejea katika somo hili inakazia dhana kwamba Mungu anapingwa kila mahali. Anakataliwa kama Bwana, Yeye ambaye ndiye wa kwanza na mkuu zaidi katika ulimwengu wote, anapingwa hata na sanamu ambazo waziabuduo wanaukana utukufu wa Mungu na Baba wa Bwana Yesu. Zaidi ya hayo, haki na ukamilifu wake vinatiliwa shaka na wale wenye mwelekeo wa kumlaumu kwa mambo yote yanayotokea katika ulimwengu huu ulioanguka. Pengine huduma kuu kabisa ya wale walioitwa na Bwana ni hitaji lao la kuweka wazi kwa watu wa kisasa kile ambacho Maandiko yanatangaza hasa juu ya Mungu, Yeye ni nani, anafanya nini ulimwenguni, nia yake ni nini, jinsi anavyotenda kazi, na kusudi lake kuu kwa uumbaji wake. Kichwa cha somo hili na sehemu hii, “Fundisho kuhusu Mungu na Kuenea kwa Ufalme” kinatafuta kwa uwazi kuunganisha uhusiano kati ya Mungu kama yule anayefunua utawala na utukufu wake katika ulimwengu, na nafsi yake. Kwa maneno mengine, kinatafuta kusisitiza kwamba Ufalme wa Mungu (Utawala wa haki wa Mungu juu ya ulimwengu) una uhusiano wa moja kwa moja na nafsi yake, na yale anayoyafunua kwetu kuhusu mapenzi yake. Bila Yeye kujifunua kwa wanadamu tusingejua lolote kuhusu mapenzi yake, na kwa sababu hiyo, tusingeweza kuyatendea kazi. Kwa kutokujua makusudi yake na nia zake, tungezalisha tu, kama ulimwengu unavyofanya leo, misingi ya uongo ya kujenga maisha na kutafuta “mafanikio.” Kwa namna moja, hii ni njia nzuri ya kuuelewa ulimwengu, kama kiwanda kikubwa kinachozalisha mitazamo ya uongo ambayo inatoa mitindo mbadala ya maisha isiyo na maana, isiyo ya kibiblia badala ya ile iliyotayarishwa na Bwana kwa ajili yetu. 1 Yohana 2:15-17 – Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. 16 Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia. 17 Na dunia inapita, pamoja na tamaa zake, bali yeye afanyaye mapenzi ya Mungu adumu hata milele.

 5 Page 17 Mifano ya rejea

 6 Page 18

Muhtasari wa Sehemu ya 1

Katika kuwasaidia wanafunzi wako kuelewa uhusiano wa kujifunza kuhusu Mungu na maisha ya kiakili, huenda ukahitaji kutumia nukuu hizi kutoka kwa mababa wawili wa mwanzoni kabisa mwa Ukristo ambao walionya juu ya kutegemea

 7 Page 20

Muhtasari wa Kipengele I-B

Made with FlippingBook - Share PDF online