Mungu Mwana – Mwongozo wa Mkufunzi: Capstone Module 10 Swahili Mentor Guide

/ 2 3

M U N G U M W A N A

II. Mitazamomiwili yaUfunuowaKristo: KunyenyekezwanaKuinuliwa kwa Mungu Mwana (Flp. 2:5-11 kama Kielelezo cha Kristolojia)

A. Mtazamo wa kwanza: kunyenyekezwa kwa Kristo ( kushuka kwake duniani na kufa ), Flp. 2:6-8.

Chimbuko la dini ya Wakristo ni katika Yesu Masihi. Anaitwa Mwana wa Mungu Aliye Juu Zaidi. Inasemekana kwamba Mungu alishuka kutoka mbinguni. Alijitwalia na kujivika mwili kutoka kwa bikira wa Kiebrania. Na Mwana aliishi ndani ya binti wa binadamu. ~ Aristides. (c. 125, E) 9. 265. Ibid. uk. 93-94.

1. Mungu wa milele wa mbinguni katika nafsi ya Mungu Mwana alijinyenyekeza (kujifanya mtupu) kwa habari ya sifa zake za kiungu akaja duniani.

1

2. Hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho.

3. Alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu .

4. Tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu , alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, kwenye mti wa maumivu na mateso yaWarumi.

B. Mtazamo wa pili: kuinuliwa kwa Kristo ( kupaa kwake mbinguni na cheo cha ubwana ), Flp. 2:9-11.

Ewe Mungu mkuu! Ewe mtoto mkamilifu! Mwana ndani ya Baba na Baba ndani ya Mwana.... Mungu Neno, ambaye alifanyika mwanadamu kwa ajili yetu. ~ Klementi wa Aleksandria (c. 195, E) 2.215. Ibid. uk. 95.

1. Mwana wa Mungu aliyenyenyekezwa na kusulubiwa amefufuliwa katika wafu na kuinuliwa na Baba hadi kwenye nafasi ya utukufu wa milele, heshima, na mamlaka ya kutawala kama Bwana juu ya viumbe vyote.

2. Mungu alimwadhimisha mno , akimpa jina kuu kupita majina yote katika ulimwengu wote.

3. Kwa jina la Yesu kila goti litapigwa kwa utii na kujisalimisha.

Made with FlippingBook - Share PDF online