The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide
/ 2 3
UFALME WA MUNGU
b. Unapendeza kwa macho – tamaa ya macho
c. Una nguvu ya kuleta hekima - kiburi cha uzima
d. Ona uwiano sawa katika jaribu la Yesu, Mt. 4; Marko 1; Luka 4
C. Matokeo ya kutisha ya dhambi ya Adamu na Hawa: ukaidi, mgogoro na aibu, ubinafsi, kutengwa, na hatimaye, kifo.
1
Hitimisho
ukurasa 311 11
» Mungu wa Utatu ndiye Bwana mkuu, anayetawala juu ya vyote.
» Utawala wake ulipingwa kupitia uasi wa kishetani huko mbinguni, na kupitia uasi wa hiari na kutotii kwa wanadamu wawili wa kwanza duniani.
Tafadhali chukua muda mwingi uwezavyo kujibu maswali haya na mengine ambayo yaliibuka kutokana na maudhui ya video. Jibu kwa uwazi na kwa ufupi, na inapowezekana, tumia Maandiko. 1. Biblia inafafanuaje utawala na mamlaka ya Mungu Mweza wa Yote juu ya ulimwengu wote? Ni nini maana ya neno “enzi”? 2. Wanatheolojia wanaposema kwamba Mungu wa Biblia “anajitegemea,” wanamaanisha nini? 3. Kwa nini ni muhimu kwetu kufundisha, kulingana na madai ya Biblia yenyewe, kwamba Mungu aliumba ulimwengu ex nihilo ? 4. Kulingana na Maandiko, enzi kuu na utawala wa Mungu unaenea kwa umbali gani duniani kote, na katika ulimwengu wote? Eleza jibu lako. 5. Unaweza kufafanuaje “kanuni kuu ya uasi wa Shetani” katika ulimwengu? 6. Video ilionyeshaje “nia kuu ya utendaji wa kishetani”? Je, unakubaliana na kauli hii? Kwa nini ndiyo au kwa nini hapana?
Sehemu ya 1
Maswali kwa Wanafunzi na Majibu
ukurasa 311 12
Made with FlippingBook Learn more on our blog