The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide

/ 2 5

UFALME WA MUNGU

I. Matokeo ya kwanza ya Anguko, kuibuka kwa kosmos : neno la Kiyunani likimaanisha “muundo huu wa dunia ya sasa na mfumo wa uasi na dhambi.”

Muhtasari wa Sehemu ya 2 ya Video

ukurasa 312  14

A. Anguko limezaa kosmos , mfumo wa sasa wa ulimwengu usiomcha Mungu ambao unafanya kazi kulingana na kanuni za uasi zilizouanzisha.

1. Inafanya kazi chini ya mamlaka ya moja kwa moja ya shetani, chini ya udhibiti wake wa moja kwa moja, Mt. 4:8-10.

1

2. Dunia yote iko chini ya utawala wa yule Mwovu, 1 Yoh. 5:19.

3. Roho Mtakatifu anayekaa ndani ya waamini ni mkuu kuliko yule (Shetani) aliye katika dunia, 1 Yoh. 4:1-4.

B. Shetani, akiwa adui mkuu wa Mungu, anadhibiti mfumo huu wa dunia kupitia pupa, tamaa, na kiburi.

1. Eneo lililojaa uasi, majaribu, na ukosefu wa haki.

2. Mfumo ulio katika mgogoro wa kina, unaoendelea na Mungu.

3. Muundo ambao Mungu mwenyewe siku moja atauhukumu na kuuharibu.

4. Ghadhabu ya Mungu dhidi ya mfumo wa dunia ya sasa, Yakobo 4:4.

C. Falme na mamlaka: miundo na matabaka ya upinzani na dhambi.

ukurasa 313  15

Made with FlippingBook Learn more on our blog