The Kingdom of God, Swahili Mentor Guide
6 4 /
UFALME WA MUNGU
* Ni kwa kiwango gani tunaweza kumwomba Mungu afanye kazi zile zile ndani yetu na kupitia kwetu ambazo alifanya ndani ya Yesu, ikiwa mamlaka ya ufalme iko katikati yetu leo? * Kwa nini ni Wakristo wachache na makanisa machache sana yanayoishi mlipuko wa mamlaka na nguvu za utawala wa Mungu ikiwa Yesu kwa namna fulani halisi alianzisha utawala wa Mungu? * Wakristo hawakubaliani sana kuhusu unabii na mafundisho ya nyakati za mwisho. Fundisho hili la Ufalme linasaidiaje kutatua tofauti hizo au hata kufanya kuwa vigumu zaidi kuelewa fundisho la Biblia kuhusu nyakati za mwisho? Ndugu mmoja Mkristo mwaminifu, baada ya kusikia fundisho kwamba Ufalme wa Mungu tayari upo, alilichukulia kumaanisha kwamba nguvu zote za ufalme na baraka zake zinapatikana kwa ajili yetu leo. Mara moja alianza kufundisha katika darasa lake la shule ya Jumapili kwamba Yesu ameleta Ufalme, na kwa hiyo hatupaswi tena kuingiliwa au kupigwa na shetani. Hasa, alianza kuwafundisha vijana kwamba hawakupaswa tena kuwa wagonjwa, au kukosa pesa, au kutenda dhambi, au hata kukata tamaa kihisia. Kama matokeo ya mafundisho yake, migawanyiko ilizuka kati ya vijana na wazazi wao. Wengine walimuunga mkono ndugu huyo, huku wengine wakithibitisha kwamba “katika ulimwengu tutakuwa na dhiki.” Pande zote mbili zimeenda kwenye Biblia na zimekazia Maandiko hayo ambayo yanaunga mkono hoja zao; kwamba tuna ushindi katika Kristo, au, kwamba tunashindana na kupigana katika ulimwengu huu, na mwili, shetani, na mfumo huu mwovu wa majaribu. Pande zote mbili ambazo kwa namna fulani zimefadhaishwa na kuchanganyikiwa kidogo, wanakuuliza uje na kufafanua maana ya “tayari” katika Ufalme ambao upo “tayari / na bado”. Je, ungeusaidiaje ushirika huu unaotaabika kufikia uelewa wa maana halisi ya neno “tayari” na “bado” kuhusiana na Ufalme wa Mungu? Ugunduzi Uletao Ushindi
MIFANO
2
1
ukurasa 327 14
Kila Kitu ni kwa Baadaye!
Katika kushiriki mafundisho ya somo hili na baadhi ya marafiki kanisani, mwanafunzi mhitimu mgeni wa seminari inayojulikana sana anaanza kusema jinsi mtazamo huu ni wa uzushi. Akiwa anaamini sana kwamba maisha na mamlaka yote ya ufalme yameahirishwa hadi enzi zijazo, mwanafunzi aliyehitimu anaanza kuelezea jinsi Israeli walivyopewa ofa ya ufalme lakini wakaikataa, na kumuua
2
Made with FlippingBook Learn more on our blog