The Kingdom of God, Swahili Student Workbook

1 0 0 /

UFALME WA MUNGU

Kiongozi huyu aliamini ilikuwa muhimu kwa Wakristo kuelewa mambo haya, kwa kuwa yanawakilisha mambo muhimu zaidi katika maisha ya Kikristo. Mwalimu mwenzake hakukubaliana na hoja hiyo, akisema kwamba ingawa mafundisho ya Biblia juu ya mambo ya mwisho yana mahali pake, ni muhimu zaidi kuzungumza juu ya upendo na imani, mambo muhimu sana kwanza, kabla ya mazungumzo yoyote ya unabii na mambo yajayo. Una maoni gani kuhusu maoni yao, na ungesuluhishaje mazungumzo haya, ukiendelea kukazia ifaavyo fundisho la Biblia kuhusu mambo ya mwisho, na jinsi utawala wa Mungu unavyotenda kazi leo?

Kukamilishwa kwa Utawala wa Mungu Sehemu ya 1

YALIYOMO

Mch. Dkt. Don. L. Davis

Tunakusudia kufafanua eskatolojia na umuhimu wake, kuelezea kwa ufupi dhana ya kibiblia ya kifo, na kisha kujadili pamoja mafundisho ya Biblia juu ya hali ya wafu. Malengo yetu ya sehemu hii ya kwanza ya Kukamilishwa kwa Utawala wa Mungu ni kukuwezesha: • Kufafanua na kuelewa umuhimu wa fundisho la mambo ya mwisho ( eskatolojia ) katika Maandiko, na uhusiano wake na ufuasi na maisha ya Kanisa. • Kueleza kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu kifo, kwa Mkristo na asiye Mkristo. • Kukariri kile ambacho Maandiko yanafundisha kuhusu hali ya wafu, kipindi cha kati ya kifo cha mtu mmoja-mmoja na mwisho wa wanadamu wote kwenye utimilifu wa Ufalme wa Mungu.

Muhtasari wa Sehemu ya 1

4

I. Ufafanuzi wa eskatolojia

Muhtasari wa Sehemu ya 1 ya Video

A. Eskatolojia, Kiyunani cha “elimu ya mambo ya mwisho”

B. Kwa nini ni lazima tuwe na bidii na umakini kujifunza matukio na kweli zinazohusiana na kuja kwa Bwana wetu tena? Kuna sababu mbili zinazotolewa:

Made with FlippingBook - Online catalogs