The Kingdom of God, Swahili Student Workbook
/ 1 9 5
UFALME WA MUNGU
Ufalme Wako Uje! Usomaji kuhusu Ufalme wa Mungu (muendelezo)
Ndege waliruka kwenye miti. Tulizungumza kuhusu amani, wakati ujao na Ufalme wa Mungu. Kwa namna fulani, licha ya tofauti zetu za umri na uelewa, sote wawili tulihisi kwamba Mungu anataka amani na kwamba ataleta kile anachotaka. Siku moja, tulisema na tulijua, ulimwengu wote utakuwa kama wakati huu wa ajabu. Lakini haitatokea bila gharama na mapambano. Yesu anahimiza hivi: “Ingieni kupitia mlango mwembamba.” Maana “mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache” (Mathayo 7:13-14). Ufalme wa Mungu ni uzima tele (Yohana 10:10), lakini njia ya uzima ni kupitia mlango mwembamba wa imani na utii kwa Yesu Kristo. Ikiwa Wakristo leo wanataka kujionea mfumo wenye amani wa Ufalme, ni lazima wajifunze na kuiishi njia ya Mungu ya amani. 1. Jambo muhimu zaidi maishani ni kuwa mfuasi wa Yesu Kristo. Ili kufanya hivyo ni lazima tujifunze kutoka kwake na kutii yale tunayosikia. Ni lazima awe Mwalimu wetu na Bwana wetu (Mt 7:24-27; 11:29; 28:18-20; Yoh. 13:13 ). 2. N i wazi kwamba hatuwezi kumfuata Yesu ikiwa hatujui alichofundisha. Mada kuu ya mahubiri na mafundisho yake ilikuwa ni Ufalme wa Mungu. Wakristo wengi hawalijui hili, hata hivyo bado wanamwita Bwana na Mwalimu Mkuu! 3. L akini baada ya hapo, tunakabiliwa na tatizo la papo hapo. Mara tu tunapojua mada kuu ya mafundisho yake, moja kwa moja tunaielewa vibaya. Ufalme unamaanisha kitu tofauti katika nahau ya Biblia (Kiebrania, Kiaramu, Kiyunani) kuliko katika Kiingereza cha kisasa. Kwetu “Ufalme” maana yake ni “eneo” (himaya ambapo mfalme anatawala) au “kundi la watu wanaoishi katika milki ya mfalme” (watu ambao mfalme anawatawala). Hata hivyo, katika Biblia maana kuu ya “Ufalme” ni “utawala” au “mamlaka.” Kwa hiyo Ufalme wa Mungu unamaanisha utawala wa Mungu au mamlaka ya Mungu. Ufalme wa Mungu si mahali wala watu, bali ni utawala wa Mungu unaofanya kazi na wenye nguvu. Ufalme ni tendo la Mungu, yaani, jambo analofanya. 4. M zigo na madhumuni ya huduma ya Yesu ya miaka mitatu kabla ya kifo na ufufuo wake ilikuwa ni kuhubiri, kutangaza na kufundisha kuhusu Ufalme wa Mungu (Mk. 1:14-; Mt. 4:17, 23; 9:35; Lk 4:42; 8:1; 9.2, 6, 11; 10:1, 9; Mdo 1:3; 28:31). Mahubiri na Mafundisho ya Yesu Muhtasari wa Mafundisho, Vic Gordon
Made with FlippingBook - Online catalogs