The Kingdom of God, Swahili Student Workbook

/ 3 5

UFALME WA MUNGU

kwa Utawala wa Mungu ”? Ni maarifa gani yanaweza kutusaidia kuelewa vyema zaidi ukweli huu wa hali za miji na majiji?

Mauaji ya Kimbari ya Wayahudi katika Vita vya Pili vya Dunia

Wakati wa Vita vya Pili vya Dunia, zaidi ya Wayahudi milioni sita waliuawa wakati wa vita vya Ulaya. Mamia ya maelfu ya watoto na watoto wachanga wasio na hatia walichinjwa kwa sababu ya kampeni ya kiwendawazimu ya Hitler ya kuwaondoa watu wote wa asili ya Kiyahudi ulimwenguni – wanaume wazee, wanawake, wavulana, wasichana, vijana, watu wa makamo – mtu yeyote wa urithi wa Kiyahudi. Tunawezaje kusema kwamba Mungu ndiye anayetawala wakati mamilioni mengi sana ya watu wasio na hatia wameteswa na kuuawa bila sababu, kama katika mfano huu mbaya wa Wayahudi? Katika kitabu cha Danieli, tunaona mtakatifu huyu mcha Mungu akimwomba Mungu kwa niaba ya wana wa Israeli. Kama unavyokumbuka, watu wa Israeli walikuwa utumwani kwa sababu ya ukosefu wa haki na ibada ya sanamu waliyokuwa wakifanya hapo awali, na, kama matokeo ya adhabu ya Mungu, aliruhusu watu wake wapelekwe utumwani. Katika maombi ya kina ya maombezi (ona Danieli 10), Danieli anamtafuta Mungu baada ya majuma matatu ya maombolezo. Anatembelewa na malaika ambaye anamwambia kwamba haimpasi kuogopa, kwa sababu tangu siku ya kwanza ambayo alikuwa ameweka moyo wake katika kulielewa hili na juu ya kujinyenyekeza mbele za Mungu maneno yake yalisikiwa, na kwamba yeye, malaika, alikuja kwa ajili ya kuleta majibu ya maombi ya Danieli. Hata hivyo, “mkuu wa ufalme wa Uajemi alinipinga siku ishirini na moja; bali, tazama, huyo Mikaeli, mmoja wa hao wakuu wa mbele, akaja kunisaidia; nami nikamwacha huko pamoja na wafalme wa Uajemi” (ona Danieli 10:12-14). Wengi wanaamini kwamba hii ni dondoo kuhusu aina ya vita vya kiroho vinavyotuzunguka, visivyoonekana lakini vyenye nguvu na halisi. Je, una maoni gani kuhusu mfano huu muhimu lakini wenye utata? Je, kifungu kama hiki kinasaidia au kuzuiaje uelewa wetu wa kupingwa kwa utawala wa Mungu leo? Upinzani kwa Maombi ya Danieli katika Danieli 9-10

2

1

3

Mungu, kama Bwana, anatawala juu ya vyote, lakini utawala wake ulipingwa kupitia uasi wa kishetani huko mbinguni, na kupitia uasi wa hiari na kutotii kwa wanadamu wawili wa kwanza duniani. Upinzani huu, unaojulikana kitheolojia kama “Anguko,” umesababisha laana juu ya uumbaji, na kusababisha uharibifu

Marudio ya Tasnifu ya Somo

Made with FlippingBook - Online catalogs