Theology of the Church, Swahili Mentor Guide
/ 9 1
THEOLOJIA YA KANISA
g. Eze. 33:11
3. Mungu kibinafsi huchagua watu binafsi kwa ajili ya wokovu, akihakikisha milele ukombozi wao wa hakika na uliobarikiwa.
ukurasa 248 5
a. Mungu amehakikisha wokovu wa watu wake mwenyewe kupitia uwezo wake wa kujua mambo yajayo na uamuzi wake kwa habari ya maisha, Rum. 8:28-30.
b. Mungu amewachagua wale wanaomwamini Yesu Kristo kwa ajili ya wokovu, kuwa wanufaika wa uzima wake wa milele, Efe. 1:4-6.
c. Wote ambao Baba humpa Yesu watakuja kwake, Yoh. 6:37; na hakuna awezaye kuja kwa Kristo isipokuwa amevutwa na Baba, Yoh 6:44.
3
d. Alituchagua na kutuweka ili tuzae matunda yanayodumu (Yoh. 15:16).
C. Mjadala huu wa makusudi ya Mungu ya kuchagua unazaa kanuni kadha wa kadha.
ukurasa 248 6
1. Kwanza, rehema ya Mungu haitolewi kwa msingi wa jitihada na sifa za kibinadamu, bali kwa msingi wa fadhili na neema ya Mungu pekee; Kutoka 33:19 imenukuliwa katika Warumi 9:15-16.
ukurasa 250 7
2. Pili, uchaguzi wa Mungu unafanywa kwa msingi wa kusudi lake kuu kwa namna ambayo hakuna mtu anayeweza kujivunia haki au utakatifu wake mwenyewe, Efe. 2:8-9.
Made with FlippingBook - Share PDF online