Theology of the Church, Swahili Student Workbook

1 2 /

THEOLOJIA YA KANISA

• Inafuata muhtasari au mpangilio uliotolewa hapo juu, na imeandikwa kwa namna ambayo msomaji ataweza kuelewa. • Inaonyesha jinsi kifungu husika kinavyohusiana na maisha na huduma leo. Usiruhusu maagizo haya yakuogopeshe; hii ni kazi ya kujifunza Biblia! Unachohitaji kuonyesha katika kazi hii ni kwamba ulisoma andiko husika, umeeleza kwa muhtasari maana yake, ukaweza kupata kanuni chache muhimu kutoka katika andiko hilo, na kuzihusianisha na maisha na huduma yako mwenyewe. Kazi ya ufafanuzi inabeba alama 45 na inawakilisha 15% ya jumla ya maksi zako, hivyo hakikisha kwamba unaifanya kazi yako kuwa bora na yenye maarifa ya kutosha ya Neno la Mungu. Neno la Mungu li hai na linafanya kazi, na hupenya hadi kwenye kiini cha maisha yetu na mawazo ya ndani kabisa (Ebr. 4:12). Mtume Yakobo anaweka msisitizo zaidi juu ya kuwa watendaji wa Neno la Mungu, sio wasikiaji tu, tukijidanganya wenyewe. Tunahimizwa kulifanyia kazi, kulitii. Anaongeza kusema kwamba kupuuza nidhamu hii ni sawa na sisi kujitazama sura zetu za asili katika kioo na mara tunapoondoka tunasahau asili yetu (sis ni nani) na tulichokusudiwa kuwa. Katika kila hali, mtendaji wa Neno la Mungu atabarikiwa katika kila atendalo (Yak. 1:22-25). Shauku yetu ya dhati ni kwamba uweze kutumia maarifa unayojifunza kwa vitendo, ukiihusianisha elimu hii na masuala na mahitaji halisi katika maisha yako binafsi, na huduma yako ndani ya kanisa lako na kupitia kanisa lako. Kwa hivyo, sehemu hii muhimu ya kukamilisha moduli hii itakuhitaji kubuni kazi ya huduma kwa vitendo ili kukusaidia kushirikisha wengine baadhi ya maarifa ambayo umejifunza katika kozi hii. Andiko la 1 Petro 2:9-10 linalielezea Kanisa kama taifa, ukuhani, na watu. Hakuna neno lolote kati ya haya linaloturuhusu kuuelewa wokovu wetu kama suala la mtu binafsi lisilohusiana na kusanyiko. Lengo la kazi hii ya huduma kwa vitendo ni kukusaidia kuimarisha ujuzi wako katika kuelezea uhusiano kati ya wokovu na Kanisa. Tafadhali kamilisha kila moja ya hatua zifuatazo: Tambua na uelezee kwa ufupi kwa maandishi hali fulani katika uzoefu wako wa zamani au wa sasa ambapo mtu unayemjua anadai kwamba hafikirii Kanisa kuwa ni sehemu muhimu ya maisha yake ya kiroho. (Unaweza kutumia jina la kubuni kwa ajili ya mtu huyu ikiwa ungependelea kuficha utambulisho wake). Namna hii ya kuliupuuzia Kanisa inajidhihirisha katika maneno yake; “Sijisikii kama ni Kazi ya Huduma

Utoaji Maksi

Dhumuni

Mpangilio na Muundo

Hatua ya Kwanza

Made with FlippingBook flipbook maker