Theology of the Church, Swahili Student Workbook

/ 1 3

THEOLOJIA YA KANISA

lazima niende kanisani ili kumwabudu Mungu!” Au inaweza kujionyesha katika tabia yake; anadai kuwa ni mkristo mzuri lakini mahudhurio yake kanisani ni ya mara chache sana. Andika mfano wa barua kwa mtu huyu ukianisha kwa maneno yako mwenyewe sababu ambazo zinakufanya uamini kwamba ameelewa vibaya kile ambacho Biblia inafundisha kuhusu wokovu na Kanisa. Maudhui ya barua hiyo yanapaswa kutokana na theolojia ambayo umejifunza katika kozi hii, na yaonyeshe ufahamu wako wa theolojia hiyo. Lengo la barua hii ni kuhamishia mawazo na dhana za kitheolojia katika uzoefu wa kivitendo. Hili si “andiko la kitheolojia,” bali ni wasilisho la mafundisho ya kibiblia ya kweli kwa mtu ambaye anaonyesha kuwa na uelewa potofu wa Maandiko au ameamua kwa makusudi kuyaasi Maandiko. Kabidhi nakala ya barua kwa mwalimu wako. Kisha, tafakari katika maombi ikiwa Mungu anaweza kukuruhusu umfikie mtu uliyeandika habari zake (ikiwa ni jambo lililopo sasa) na umtumie barua hiyo au kuzungumza naye ana kwa ana kuhusu wokovu wake na maisha ya kanisa. Kazi ya huduma inabeba alama 30 ambazo zinawakilisha 10% ya jumla ya maksi zako, hivyo hakikisha unashirikisha yale uliyojifunza kwa ujarisi na ripoti yako iwe yenye kueleweka vizuri.

Hatua ya Pili

Hatua ya Tatu

Utoaji maksi

Made with FlippingBook flipbook maker