Theology of the Church, Swahili Student Workbook

1 8 /

THEOLOJIA YA KANISA

Lengo letu katika sehemu hii ya kwanza ya Ufunuo Kivuli wa Kanisa katika Mpango wa Mungu ni kukuwezesha kuona kwamba: • Kanisa lilifunuliwa tangu awali katika kusudi kuu la Mungu la kujitukuza mwenyewe kupitia jamii mpya ya wanadamu watakaoishi pamoja naye milele. • Kanisa lilifunuliwa awali katika ahadi ya Mungu ya kuwajumuisha Wamataifa katika mpango wake wa ukombozi kwa ulimwengu. • Kanisa lilifunuliwa awali katika jitihada za Mungu za kujitengenezea watu ( laos ) watakaoishi kwa ajili yake kama watu wake wa pekee. • Mungu anafanya kazi kupitia historia ya wanadamu ili kujichagulia watu wake kutoka katika mataifa yote duniani.

1

I. Kanisa la Yesu Kristo lilifunuliwa awali katika mpango wa Mungu uliotukuka: Kujiletea utukufu kupitia jamii mpya ya wanadamu, kulingana na tangazo la awali la Injili katika Agano na Ibrahimu.

Muhtasari wa Sehemu ya Kwanza ya Video

A. Kusudi kuu la Mungu ni kuliletea heshima Jina lake.

1. Uumbaji wote ulifanyika kwa mapenzi yake na kwa nguvu zake, na kwa ajili ya utukufu wake.

a. Kut. 20:11

b. Isa. 40:26-28

c. Yer. 32:17

2. Mwandishi wa Zaburi anasema kwamba ilikuwa kwa utukufu wake Mungu alipochagua na kutekeleza mpango wake wa ukombozi kwa watu wake Israeli na kuwashinda adui zake katika mpango wake, Zab. 135:8-12.

Made with FlippingBook flipbook maker