Theology of the Church, Swahili Student Workbook

/ 1 9

THEOLOJIA YA KANISA

B. Agano la Mungu na Ibrahimu: Kupitia yeye, jamaa zote za dunia zitabarikiwa, Mwa. 12:1-3. Andiko hili linafunua kwa uwazi kwamba:

1. Kupitia uzao wa Ibrahimu, jamaa zote za dunia zitabarikiwa.

2. Ahadi hii itatimizwa kwa kazi ya Mungu ya kiungu kupitia ukoo wa Ibrahimu.

1

C. Agano hili lilidhihirisha mpango wa Mungu uliotukuka wa kujichagulia watu kutoka duniani kote kwa ajili yake, wakiwemo Wamataifa, wote wakikombolewa kupitia Mwanawe, Yesu Kristo, Gal. 3:6-9. Andiko hili lina maana kadhaa muhimu kuhusu jinsi Kanisa lilivyofunuliwa kupitia agano la Ibrahimu.

1. Imani ya Abrahamu ilihesabiwa kuwa haki.

2. Waamini wanaunganishwa na ahadi ya Mungu kwa Ibrahimu.

3. Maandiko yaliona mbele kwamba Mungu angewahesabia mataifa haki kwa imani katika agano la Ibrahimu.

II. Kanisa lilifunuliwa tangu awali kupitia mpango wa Mungu unaoendelea kufunuliwa: Katika Yesu Kristo, Mungu amefunua siri yake kwa ulimwengu wote kuhusu nia yake ya kujitengenezea watu kwa utukufu wake miongoni mwa Wayahudi na mataifa. Maandiko matatu yanayoonyesha wazi wazi ufunuo wa siri ya Mungu ya kuwakomboa mataifa kupitia ahadi yake kwa Ibrahimu.

Made with FlippingBook flipbook maker