Theology of the Church, Swahili Student Workbook

2 0 /

THEOLOJIA YA KANISA

A. Andiko la Kwanza: Siri iliyofichwa kwa vizazi vingi sasa imefunuliwa kupitia manabii na mitume, Rum. 16:25-27. Andiko hili linaonyesha mambo kadhaa muhimu:

1. Siri hii: ni mahubiri ya Injili ya Yesu Kristo.

2. Mahubiri haya ya Yesu Kristo ni kulingana na ufunuo wa siri iliyokuwa imefichwa kwa miaka mingi.

1

3. Siri hii imefunuliwa kupitia mitume na manabii kwa mataifa yote kwa ajili ya kuwaleta katika utii wa imani.

B. Andiko la Pili: Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu kama ufunuo wa siri ya Mungu, Kol. 1:25-29. Maelezo muhimu tunayojifunza kuhusu siri hii ni:

1. Siri iliyokuwa imefichwa kwa vizazi na kwa miaka mingi sasa imefunuliwa kwa watakatifu wake.

2. Mungu ameweka wazi miongoni mwa mataifa utajiri wa utukufu wa siri hii.

3. Siri hii ni Kristo ndani yenu, yaani mataifa, ambalo ni tumaini letu la utukufu.

C. Andiko la Tatu: Ufunuo wa siri ya ujumuishwaji wa mataifa katika Kanisa, Efe. 3:4-12. Siri ya Imani katika Kristo:

Made with FlippingBook flipbook maker