Theology of the Church, Swahili Student Workbook
/ 2 1
THEOLOJIA YA KANISA
1. Haikufunuliwa kwa vizazi vya zamani lakini sasa imefunuliwa kwa mitume watakatifu wa Kristo na manabii kwa njia ya Roho.
2. Ni kwamba mataifa ni warithi wenza, washirika wa mwili mmoja, na washiriki wa ahadi katika Yesu Kristo kupitia imani katika Injili.
3. Kupitia huduma ya kitume, siri ya Mungu imewekwa wazi: kwamba kupitia Kanisa, Mungu angewajulisha watawala na wenye mamlaka katika ulimwengu wa roho hekima hii kuu ya Mungu.
1
III. Kanisa lilifunuliwa kupitia Taifa la Israeli, ambapo Mungu ametupatia picha ya watu wake wa pekee, Laos wa Mungu, 2 Kor. 6:16; 2 Thes. 2:13-14.
A. Israeli ni chombo ambacho kupitia hicho Masihi angekuja.
1. Israeli ni jina alilopewa Yakobo baada ya pambano lake kuu la maombi na malaika, Mwa. 32:28.
2. Hili ndilo jina la jumla walilopewa wazawa wa Yakobo.
a. Makabila kumi na mawili yanaitwa “Waisraeli.”
b. “Wana wa Israeli,” Yosh. 3:17; 7:25; Amu. 8:27; Yer. 3:21.
c. “Nyumba ya Israeli,” Kut. 16:31; 40:38.
Made with FlippingBook flipbook maker