Theology of the Church, Swahili Student Workbook
2 2 /
THEOLOJIA YA KANISA
3. Ukoo huu wa kimwili wa Ibrahimu ulichaguliwa kwa msingi wa uaminifu wa Mungu kwa agano lake na Abrahamu, Kum. 7:6-8.
4. Uchaguzi wa Mungu na agano lake na Abrahamu, Isaka, na Yakobo viliendelea kwa kizazi chao. Masihi alipaswa kuja kupitia taifa la Israeli, na kupitia yeye, wokovu kwa ulimwengu wote.
a. Kutoka 19:5-6
1
b. Kumb. 14:2
c. Kumb. 26:18-19
d. Yohana 4:22
5. Israeli inatambulika kama watu wa Mungu: taz. Kut. 15:13, 16; Hes. 14:8; Kum. 32:9-10; Isa. 62:4; Yer. 12:7-10; Hosea 1:9-10.
6. Watu wa mataifa walifunuliwa awali kama watu wa Mungu, Rum. 9:24-26.
B. Picha ya Israeli kama watu wa Mungu sasa inatumika kwa Kanisa kama jamii ya kifalme ya agano la Mungu.
1. Kanisa, kama watu wapya wa Mungu, Wayahudi na mataifa, sasa wamekuwa watu wa Mungu, 1 Pet. 2:9-10.
a. Kanisa la Mungu halitambuliki kwa njia ya tohara bali kwa uumbaji mpya kupitia imani katika Yesu, 2 Kor. 5:17 (rej. Fil. 3:2-3).
Made with FlippingBook flipbook maker