Theology of the Church, Swahili Student Workbook
3 4 /
THEOLOJIA YA KANISA
h. Na mwishowe, wanaletwa katika nchi ya ahadi (Kanaani) yenye mji mkuu wenye utukufu (Yerusalemu), ambamo wanaishi kwa amani chini ya Mfalme mkuu (Daudi).
2. Wokovu kutoka dhambini:
a. Watu watumwa wanaoishi katika mateso bila matumaini (kila mwanadamu chini ya dhambi),
1
b. Wanaitwa na Mungu kwa uchaguzi wake wa neema kupitia Shujaa ambaye Mungu anatuma (Yesu),
c. Wanaokolewa na ghadhabu ya Mungu kwa njia ya damu (Yesu, Mwana-kondoo wa Mungu aliyechinjwa),
d. Wanaokolewa kutoka kwa mfalme mwovu kupitia nguvu kuu za Mungu (ushindi dhidi ya Shetani na majeshi yake ya mapepo),
e. Wanakombolewa kwa kupita katika maji (ubatizo),
f. Wanaundwa kuwa taifa takatifu (Kanisa) wanaotii mapenzi ya Mungu (amri za Kristo),
g. Wanapewa jukumu la kuwa mashahidi kwa mataifa (Mathayo 28:18-20),
h. Na mwishowe, wanaletwa katika nchi ya ahadi (uumbaji mpya) yenye mji mkuu wenye utukufu (Yerusalemu Mpya), ambamo wanaishi kwa amani chini ya Mfalme mkuu (Yesu).
Made with FlippingBook flipbook maker