Theology of the Church, Swahili Student Workbook
/ 3 5
THEOLOJIA YA KANISA
3. Kuokolewa katika tendo la “Kutoka” kulimaanisha nini?
4. Kuokolewa kulimaanisha nini katika Agano Jipya?
a. Rum. 8:20-25
b. 2 Pet. 3:13
1
Hitimisho
» Kuokolewa kunamaanisha kuondolewa kutoka katika hali ya upotevu na kutengwa na Mungu kunakosababishwa na dhambi kwa kuunganishwa na Kristo na hivyo kujiunga na “watu wa Mungu” wanaorithi Ufalme aliouahidi. » Wokovu huu daima unahusisha tendo la mtu katika maisha yake kuokolewa kutoka katika hukumu ya Mungu juu ya dhambi na kupata uhuru kutoka katika utumwa wa dhambi. » Wokovu na Kanisa ni kama pande mbili za sarafu moja, kwa sababu kuokolewa, kwa maana yake halisi, kunamaanisha kuwa sehemu ya watu wa Mungu. Watu hupata wokovu mmoja mmoja, lakini hakuna anayeokolewa ili kuishi maisha ya wokovu peke yake. Kuunganishwa na Kristo daima kunahusisha kuunganishwa na watu wake. » Kanisa ni sehemu ya hadithi kubwa ya Mungu ambayo itapelekea mbingu mpya na nchi mpya pamoja na jamii mpya ya wanadamu chini ya utawala wa Mungu, hali ambayo itabatilisha kabisa athari za dhambi na mauti ulimwenguni. » Kuita watu kuokolewa ni kuwaalika washiriki katika ulimwengu huo mpya kwa imani katika Yesu atakayekuwa mtawala wake.
Made with FlippingBook flipbook maker