Theolojia Katika Picha

1 5 6 /

R e p r e s e n t a n d o l a t e o l o g í a

Kutoa Utukufu kwa Mungu Mch. Dkt. Don L. Davis

Yohana 17:3-4 - Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma. 4 Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye Inashangaza jinsi tunavyoweza kutoelewa mambo. Tunafikiri tunajua kitu kinahusu nini, na tunatenda kulingana na mawazo yasiyo sahihi, na kisha tunashangazwa na jinsi mambo yanavyoenda vibaya, au tunashangaa tunapogundua kwamba tulikuwa mbali katika kufikiri kwetu. Jioni moja, binti mdogo alikuwa akisali pamoja na mama yake kabla ya kulala. “Mpendwa ‘Litukuzwe’, tafadhali mbariki Mama na Baba na marafiki zangu wote,” alisali. «Subiri kidogo», mama yake alimkatiza, «Litukuzwe ni nani?» “Hilo ni jina la Mungu,” alimjibu. “Nani alikuambia hilo ni jina la Mungu?” aliuliza mamaye. “Nilijifunza katika shule ya Jumapili, Mama. Baba yetu, uliye mbinguni, jina lako Litukuzwe.” ~ Bruce Larson Ninaamini kwamba kwa Wakristo wengi leo, maisha ya Kikristo kimsingi yanafikiriwa na kutafsiriwa vibaya. Ingawa wanaamini kwamba wana ufahamu sahihi wa mambo, wanakosea, na kama mtoto mdogo, wanaendelea na makosa yao, bila kujua kwamba ufahamu wao kuhusu kusudi la maono yote ya Kikristo umepotoka. Asubuhi ya leo tutazungumza kuhusu kusudi la mwisho ya mambo yote, na lengo kuu la dini ya Kikristo, maisha yote ya kanisa, na sababu ya kuwepo kwetu. Tupo kwa ajili ya utukufu wa Mungu!

I. Nini Maana ya Kumtukuza Mungu?

A. Kumtukuza Mungu kunamaanisha kwamba tunampa kile anachostahili; ibada ndiko huko “kustahili,” kumpa Mungu kile anachostahili kwa vile alivyo na kwa kazi yake.

Made with FlippingBook Digital Publishing Software