Theolojia Katika Picha

3 0 /

R e p r e s e n t a n d o l a t e o l o g í a

Funguo kwa Utafsiri wa Biblia Baadhi ya Funguo za Kutafsiri Biblia kwa Usahihi Terry G. Cornett na Don L. Davis. Toleo Lililopitiwa Upya

Kanuni za Msingi

Ili kupata uelewa sahihi wa kitabu au kifungu cha Maandiko toka kwenye Biblia, mtafsiri lazima: 1. A mini kwamba Maandiko yamevuviwa, hayana makosa na ni sheria yenye mamlaka kwa ajili ya maisha na Fundisho. 2. T ambua kwamba haiwezekani kuelewa kikamilifu Maandiko na kuyafanyia kazi bila: • “Kuzaliwa kutoka juu” kwa njia ya imani katika Kristo. • Kujazwa na Roho Mtakatifu wa Mungu • Kuwa na bidii kutafuta maana yake kwa njia ya kujifunza mara kwa mara. • Kuwa tayari kutii ujumbe wake, pale unapofunuliwa.

Dhana iliyopo

3. R uhusu mchakato wa utafsiri kuhusisha “utu wote”. Kujifunza Maandiko lazima kutengeneze hisia zako na nia yako pamoja na akili yako, tunatakiwa kutosikiliza zaidi hisia au mawazo yetu katika kujifunza lakini tusiwe wasomaji tusio na shauku”.

4. F ahamu kwamba Maandiko yote kwa namna fulani yanamshuhudia Kristo. Kristo ndio kiini cha Biblia; fundisho lake, mafundisho na maadili ya kiroho yanamlenga yeye.

5. Chukulia maanani pande zote za kimungu na kibinadamu katika Maandiko

6. T afuta “kutohoa” au kutoa maana ambayo iko kwenye Maandiko (exegesis) na sio kuweka kwenye Maandiko mawazo na mtazamo wa mtu binafsi (eisegesis).

Made with FlippingBook Digital Publishing Software