Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
/ 1 5
U O N G O F U & W I T O
Neno Linaloumba
S O M O L A 1
ukurasa 177 1
Karibu katika Jina lenye nguvu la Yesu Kristo! Baada ya kusoma, kujifunza, kushiriki katika mijadala, na kutendea kazi yaliyomo katika somo hili, utakuwa na uwezo wa: • Kutetea wazo kwamba Maandiko Matakatifu ni Neno la Mungu, rekodi iliyoandikwa ya Neno la Bwana lenye uzima na la milele. • Kuonyesha kutoka katika Maandiko kwamba Mungu wa Biblia, Mungu wa Utatu, anatoa uhakikisho kwamba Neno la Mungu ni la kweli, jambo ambalo linalifanya liwe na sifa ya kutegemeka kabisa. Vitu vyote katika ulimwengu viliumbwa kupitia Neno la Mungu linaloumba na kutoa uhai. • Kueleza jinsi Bwana Mungu anavyojihusianisha kikamilifu na Neno la Mungu, hasa katika Yesu Kristo, Nafsi ya Pili ya Utatu, ambaye kupitia kwake Mungu amejifunua, anaukomboa ulimwengu, na ataurudisha ulimwengu chini ya utawala wake wa haki. • Kuthibitisha kwa kutumia Maandiko kwamba Neno la Mungu, likiwa limeingiziwa uhai wa Mungu mwenyewe, ni njia ambayo Roho Mtakatifu anaumba maisha mapya kwa wale wanaoamini. • Kufafanua ukweli kwamba kupokea Neno na kudumu katika Neno hili la Mungu lililopandikizwa ndani yetu ni ishara ya kweli ya ufuasi na kufanywa wana wa kweli katika familia ya Mungu. Kama watakatifu wa Mungu, tunapokea Neno la Mungu pamoja katika jamii yake ya agano. • Kuonyesha jinsi Neno linavyofunua kusudi kuu la ulimwengu ulioumbwa, ambalo ni utukufu wa Mwenyezi Mungu. • Kunukuu kwa moyo kifungu kinachohusiana na nguvu ya uumbaji ya Neno la Mungu.
Malengo ya Somo
ukurasa 177 2
1
Kutamanika kwa Neno Hai la Mungu
Ibada
Soma Zaburi 19:7-11 . Zama zetu zinajulikana zaidi kama zama za shauku. Watu wanajibidiisha kwa nguvu kubwa kupata vitu, kupata raha, kupata vyeo, na kutimiza malengo yao, huku nyakati fulani wakijitaabisha sana kwa ajili ya mambo wanayotamani. Labda janga la kusikitisha zaidi katika maisha ya mamilioni ya watu
ukurasa 177 3
Made with FlippingBook flipbook maker