Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
1 6 /
U O N G O F U & W I T O
ni kwamba wanajitaabisha kwa mambo ambayo, mwisho wa siku, hayatakuwa na umuhimu wowote. Wanaishi kwa ajili ya raha za muda mfupi, mali, na mambo ya kibinafsi ambayo ndani ya miaka mia moja hayatakuwapo au hayatakuwa na umuhimu wowote. Ili kuishi vizuri kweli hatupaswi kuwa na shauku kubwa tu, bali lazima tuelekeze shauku na matamanio yetu katika mambo yatakayodumu, na mambo ya maana zaidi. Kwa mujibu wa Neno la Mungu, kuna vitu vichache sana vyenye sifa ya kuwa vitu vya maana sana, na kwa sababu hiyo, kuna vitu vichache tu vinavyostahili kutamanika na kutafutwa. Mojawapo ya hazina ya maana sana inayotajwa katika Maandiko ni Neno la Mungu lenyewe. Mungu anatangaza kwamba Neno lake, Neno lililoandikwa, yaani Maandiko Matakatifu, ni hazina ambayo inastahili jitihada zetu za unyoofu na bidii zaidi katika kulipata. Hakuna kitu duniani kinachodumu kama hicho; hakuna kinachoweza kutupatia hekima, ufahamu, tumaini, na shangwe ambayo Neno linatoa. Neno la Mungu ni mali yenye utajiri mwingi, hutiamacho nuru, hufurahishamoyo, huhekimisha nafsi, na kuleta tumaini katika maisha ya mtu. Mtunga-zaburi hapa anaonyesha wazi jinsi Neno lililo hai la Mungu linavyostahili kutamanika kwetu. Hakuna kitu ambacho tunamiliki au ambacho tunaweza kumiliki chenye thamani na umuhimu kama Neno la Mungu kuhusu Mwanawe, mpango wake, na tumaini letu. Katika kulishika tunaonywa, na katika kushikamana nalo kuna thawabu kubwa. Je, unatafuta Neno la Mungu kama vile unavyotafuta pesa, au raha, au muda huru wa kujiburudisha, au nafasi kubwa? Hakuna kitu katika ulimwengu huu chenye thamani au umuhimu kama ujuzi wa kina wa Neno la Mungu. Haja ya moyo wako iko wapi leo? Baada ya kutamka na/au kuimba Kanuni ya Imani ya Nikea (katika kiambatisho), sali sala ifuatayo: Mungu wa Milele, Baba yetu, tunakusifu kwa nia yako ya kujidhihirisha kwetu kupitia Neno lako. Umetubariki kwa kuhifadhi ahadi yako ya neema na matamko yako kwa njia ya Maandiko, ambayo uliyavuvia kwa Roho wako Mtakatifu. Na sasa, kwa njia ya Roho huyohuyo, unatufundisha kuhusu Mwanao, na mpango wako mtukufu wa kurejesha vitu vyote katika yeye. Tunalibariki jina lako kuu na takatifu kwa Neno lako lililo hai na la kudumu, na tunakuomba utujalie hekima yako tunapojifunza pamoja nguvu na ukuu wa Neno lako. Mungu mwenye rehema, Baba wa mbinguni, umetuambia kwa kinywa cha Mwanao mpendwa, Bwana wetu Yesu Kristo, “Mwombeni Bwana wa mavuno,” juu ya agizo lako hili la kimungu, tunaomba kutoka mioyoni mwetu, kwamba umtoe Roho Mtakatifu kwa
1
Kanuni ya Imani ya Nikea na Maombi
ukurasa 178 4
Made with FlippingBook flipbook maker