Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

/ 1 7

U O N G O F U & W I T O

wingi kwa watumishi wako hawa, pamoja nasi na wale wote walioitwa kulitumikia neno lako. Amina. ~ Martin Luther . Devotions and Prayers of Martin Luther . Trans. Andrew Kosten. Grand Rapids: Baker Book House, 1965. Uk. 77.

Hakuna jaribio katika somo hili.

Jaribio

Mazoezi ya Kukariri Maandiko

Hakuna maandiko ya kukariri katika somo hili.

1

Hakuna kazi za kukusanya katika somo hili.

Kazi za Kukusanya

MIFANO YA REJEA

Swala la Utaalamu

Katika jamii kwa ujumla leo ni jambo la kawaida kwa watu wengi walio na matatizo ya kitaaluma au ya kibinafsi kuyashughulikia wao wenyewe, au kushauriana na «wataalamu» - wanasayansi, madaktari, washauri, au wengine ambao wanachukuliwa kuwa wao wanaweza kuwawezesha kukabiliana na matatizo yao au kuyatatua. Neno la Mungu lina nafasi gani leo katika kutatua matatizo ya watu? Je, ni kwa njia gani unaona au kushindwa kuona kuheshimiwa kwa mafundisho ya Neno la Mungu katika jamii leo?

1

ukurasa 178  5

Mamlaka Iko Wapi?

Fikiria kwamba suali tata linaibuka katika kundi la huduma ya vijana ya kanisa lako la mahali kuhusu ngono kabla ya ndoa. Watoto wengi wanafundishwa katika shule zao za sekondari kwamba kujihusisha na ngono ni jambo la kawaida na linalotarajiwa, na ni sawa ilimradi wachukue tahadhari dhidi ya magonjwa ya zinaa na hatari ya kupata mimba. Hoja zinazotolewa katika shule za sekondari zinaonekana za kuvutia kwa baadhi ya wanafunzi katika kikundi chako cha vijana, ambao wanashangaa na kuhoji ni kwa namna gani viwango na kanuzi za kitabu cha kale kama Biblia zinaweza kuhusiana nao kama vijana leo. Je, unaweza kusema nini kwa watoto hao ambao wanaelekea hatua ya kukataa mamlaka ya Maandiko juu ya maisha yao, wale ambao wanazidi kusadikishwa kwamba mambo yako sawa ikiwa tutayashughulikia kwa kuwajibika na kwa uwazi?

2

Made with FlippingBook flipbook maker