Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
1 8 /
U O N G O F U & W I T O
Yesu – Ndiyo; Biblia – Hapana!
Kuna watu wengi wanaokiri utii wa kina kwa Yesu na mafundisho yake, lakini wana shida na ukweli wa Biblia. Yesu alifundisha upendo, unyenyekevu, na nia njema miongoni mwa watu; Biblia, hata hivyo, imejaa mafundisho ya ajabu kuhusu malaika, mapepo, na miujiza, mambo ambayo watu wengi wa sasa wanaona kuwa magumu au kwamba hayawezekani kuamini. Je, unafikiri inawezekana kumkubali Yesu Kristo huku, wakati huohuo, tukitilia shaka mambo fulani ya Biblia? Unaweza kusema “Ndiyo!” kwa Yesu, lakini “Hapana!” au “sina uhakika” kwa mambo mengi katika Maandiko? Je, ni lazima uamini kila kitu ambacho Biblia inafundisha ili kudai kuwa na uhusiano wa kweli na imani katika Yesu? Ikiwa jibu ni ndiyo, kwa nini? Ikiwa jibu ni siyo kwa nini?
3
1
Neno Linaloumba Sehemu ya 1
YALIYOMO
Mch. Dkt. Don L. Davis
Maandiko Matakatifu ni Neno la Mungu, kumbukumbu ya maandishi ya Neno la Bwana lenye uzima na la milele. Mungu wa Biblia, Mungu wa Utatu, anatoa uhakikisho kwamba Neno la Mungu ni la kweli, jambo ambalo linalifanya liwe na sifa ya kutegemeka kabisa. Vitu vyote katika ulimwengu viliumbwa kupitia Neno la Mungu linaloumba na kutoa uhai. Bwana Mungu anajihusianisha kikamilifu na Neno la Mungu katika Yesu Kristo, Nafsi ya Pili ya Utatu, ambaye kupitia kwake Mungu anajifunua, anaukomboa ulimwengu, na atarudisha ulimwengu chini ya utawala wake wa haki. Lengo letu la sehemu hii ya kwanza ya Neno Linaloumba ni kukuwezesha kuona, kutambua, na kuelewa maana ya jinsi ambavyo: • Maandiko Matakatifu, Neno la Mungu lililo hai na la milele, yanahusianishwa moja kwa moja na nafsi ya Mungu na kazi yake. Kwa hiyo, ni ya kutegemewa kabisa na yenye mamlaka katika yote yaliyomo ndani yake. • Ulimwengu wote mzima na uhai wote uliomo uliumbwa kupitia nguvu zinazotoa uhai za Neno la Mungu. • Mungu anajihusianisha kikamilifu na Neno la Mungu, hasa katika nafsi ya Pili ya Utatu, ambaye kupitia kwake Mungu amejifunua, anaukomboa ulimwengu, na ataurudisha ulimwengu chini ya utawala wake wa haki.
Muhtasari wa Sehemu ya 1
Made with FlippingBook flipbook maker