Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

/ 1 9

U O N G O F U & W I T O

I. Maandiko ni Neno la Mungu Aliye Hai, Limevuviwa kwa Pumzi Yake na Kuhusishwa na Nafsi na Kazi Yake.

Muhtasari wa Sehemu ya 1 ya Video

A. Maandiko ni Neno lililo hai na la milele linaloishi na kudumu milele.

1. Neno la Mungu ni la milele, lina sifa ya Mungu ya ukweli kamili na mamlaka, 1 Pet. 1:23-25.

1

2. Maandiko yamevuviwa kwa “pumzi” ya Mungu Mwenyezi.

a. 2 Tim. 3:16-17

b. Mungu alipulizia uhai wake wa uumbaji katika Neno lake.

3. Si lazima kuamini kwamba Mungu alielekeza kila kilichopaswa kuwekwa katika Maandiko ili yawe yamevuviwa na Yeye. Badala yake, tunaamini kwamba Roho Mtakatifu alitumia misamiati, uzoefu, na uwezo wa waandishi kwa njia mahususi aliyokusudia ili matokeo ya uandishi wao yawe ni kazi yake mwenyewe. Roho alivuvia maandiko kwa namna ambayo anaweza kuitwa mwandishi wa nyaraka husika. Ni kwa msingi huu Kanisa limeyahesabu Maandiko kuwa kiwango chenye mamlaka na mwongozo unaotegemeka kwa habari ya imani na utendaji (maisha).

a. 2 Pet. 1:19-21

b. Watu walinena yaliyotoka kwa Mungu huku wakiongozwa na Roho Mtakatifu mwenyewe.

Made with FlippingBook flipbook maker