Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
2 0 /
U O N G O F U & W I T O
B. Kwa sababu yamevuviwa na Mungu, haiwezekani, kwa msingi huo, Maandiko kumrudia bure, tupu, au bila matokeo. Kwa kila njia, Neno la Mungu linaonekana kuwa lenye kutegemeka kabisa na lenye mamlaka kabisa, linalostahili kutumainiwa na kujifunza.
1. Isa. 55:8-11
a. Njia za Mungu ziko juu kabisa ya njia zetu, yaani, zaidi ya utafiti au ugunduzi wetu.
1
b. Neno la Mungu linafaa kabisa katika yote ambayo Mungu analiagiza na kuliamuru lifanye.
2. Mungu anathibitisha uhakika kamili wa Neno lake takatifu, Isa. 44:26-28.
a. Mungu anatangaza kwamba atalithibitisha neno la mtumishi wake na kutimiza shauri la wajumbe wake. Neno lake ni kweli.
b. Mungu huthibitisha Neno lake kwa uhakika na uaminifu wa kweli. Kama Yesu alivyosema katika Yohana 10:35, “Maandiko hayawezi kutanguka.”
C. Kwa sababu ya kutegemeka kwake kikamilifu, Neno linaadhimishwa na kusifiwa kila mahali katika Biblia.
1. Linasifiwa kwa umilele wake kamili, Mt. 5:18.
2. Linasifiwa kwa namna ambayo Mungu analitukuza Neno lake, Isa. 42:21.
Made with FlippingBook flipbook maker