Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

/ 3 1

U O N G O F U & W I T O

e. Tunapaswa kulisikia likihubiriwa na kufundishwa katika Kanisa. Hatupaswi kudharau unabii, bali lisikie Neno kwa maana, kama Warumi 10:17 inavyodokeza, “imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa Neno la Kristo.”

f. Tunapaswa kulijumuisha katika maisha na mazungumzo yetu yote . Neno linaloumba lazima liwe nguvu inayotawala maishani mwetu kama inavyosemwa katika maneno ya Shema, Kum. 6:4-9.

1

C. Neno hili la uumbaji la Mungu lazima lisikike na kupewa utii katika mazingira ya jumuiya ya Kikristo.

1. Msidharau unabii, wala msimzimishe Roho Mtakatifu; 1 Thes. 5:19-22.

2. Neno litakuja katikati ya kusanyiko, 1 Kor. 14:26.

3. Mungu amelipatia Kanisa wanaume na wanawake waliopewa vipawa maalum na Roho Mtakatifu ili kufundisha Neno la Mungu, Efe. 4:11-13.

III. Neno Hufunua Kusudi la Milele la Mungu kwa Ulimwengu: Ili Vitu Vyote Vipate Kumpa Utukufu na Heshima kama Bwana.

A. Kuna pigo moja muhimu zaidi kutoka kwenye moyo wa Hadithi ya Kiungu: Vitu vyote viliumbwa ili kuleta utukufu, heshima, na sifa kwa Bwana na Jina lake tukufu.

1. Vitu vyote viliumbwa kwa kusudi la Mungu lililokusudiwa, Mit. 16:4.

Made with FlippingBook flipbook maker