Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi

3 0 /

U O N G O F U & W I T O

1. Waamini wanapaswa kutamani maziwa yasiyogoshiwa ya Neno la Mungu ili waweze kukua wanapojilisha, 1 Pet. 2:2.

2. Paulo, katika changamoto yake kwa wazee wa Efeso, aliwaweka katika mikono ya Mungu, na kwa Neno la neema yake “ambalo laweza kuwajenga na kuwapa urithi pamoja nao wote waliotakaswa,” Mdo 20:32.

3. Wakolosai wanahimizwa kuruhusu Neno la Mungu likae kwa wingi ndani yao, Kol. 3:16.

1

4. Paulo anampa Timotheo agizo lenye mamlaka la kujifunza ili kujionyesha kuwa mtenda kazi aliyekubaliwa na Mungu anapokuwa akilitumia (kuligawa) Neno la kweli kwa usahihi, 2 Tim. 2:15.

5. Kuna njia nyingi za kudumu katika Neno la Mungu.

a. Tunapaswa kulisoma . Ufunuo 1:3 inaahidi baraka kwa wale wanaosoma Neno la Mungu.

b. Tunapaswa kulikariri . Katika Zaburi 119:11 Daudi anasema amelificha Neno la Mungu moyoni mwake ili asije akamtenda Bwana dhambi.

c. Tunapaswa kulitafakari . Zaburi 1:3 inasema kwamba mcha Mungu hutafakari na kutafuna Neno la Mungu mchana na usiku.

d. Tunapaswa kulichunguza . Waberoya wanaitwa “watu waungwana zaidi” kuliko Wathesalonike katika Matendo 17:11 kwa sababu hawakusikia tu maneno ya Mtume Paulo, bali walichunguza Maandiko kila siku ili kuthibitisha Injili ya Paulo.

Made with FlippingBook flipbook maker