Uongofu na Wito, Swahili Module 1 Mwongozo wa Mkufunzi
6 /
U O N G O F U & W I T O
Mungu humkomboa na kumwokoa mwamini na adhabu, nguvu, na uwepo wa dhambi. Tunapogeuka kutoka dhambini na kumgeukia Mungu katika Kristo, Neno hutuongoza kupokea asili mpya ya Mungu (kuzaliwa upya) na kuingizwa (kuasiliwa) katika kusanyiko la watu wa Mungu (yaani laos ya Mungu) kwa neema kwa njia ya imani pekee. Neno linalotuita kuingia katika wokovu pia linatuita kwenye uanafunzi (kama watumwa wa Yesu), kwenye uhuru (kama watoto waliokombolewa) na utume (kufanya wanafunzi kupitia ushuhuda wetu na matendo yetu mema). Kwa kweli, Maandiko Matakatifu ni Neno linalofaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa apate kutenda kila tendo jema (2 Tim. 3:16-17). Mungu akubariki unapochunguza utajiri wa Neno lake alilolivuvia kwa pumzi yake, linaloumba, linalothibitisha, linalogeuza na linaloita!
- Mch. Dkt. Don L. Davis
Made with FlippingBook flipbook maker