Wito Halisi: Kumwakilisha Kristo na Ufalme wake kupitia Kanisa
Kuhusu Mwandishi
Mch. Dkt. Don L. Davis ni Mkurugenzi wa Urban Ministry Institute. Alipata Shahada ya Sanaa (B.A.) katika Masomo ya Biblia kutoka chuo cha Wheaton, Shahada ya Umahiri (M.A.) katika Theolojia ya Utaratibu kutoka shule ya Uzamili ya Wheaton, na ana Shahada ya Uzamivu (Ph.D.) katika Theolojia na Maadili kutoka Chuo Kikuu cha lowa Kitivo cha Dini. Dkt. Davis amefundisha kama profesa wa dini na theolojia kwenye vyuo na seminari kadhaa, ikiwemo chuo cha Wheaton, Chuo Kikuu cha Mt. Ambrose, na Chuo cha Shahada za Juu za Theolojia cha Houston. Tangu mwaka 1975, ametumika na World Impact, ambayo ni shirika la kimisheni lisilofungamana na dhehebu moja, na lililojikita katika uinjilisti, ufuasi, na upandaji wa makanisa mijini katika miji ya Marekani. Don ni mzungumzaji wa mara kwa mara katika makongamano na mikutano ya kitaifa, na anatumika pia kama Makamu wa Raisi wa Maendeleo ya Uongozi wa World Impact. Ni mhadhiri wa Staley na mwanachama wa American Academy of Religion. Kwa miaka mingi Dkt. Davis ameandika mitaala, kozi na nyenzo nyingi zilizotengenezwa ili kuwaandaa wachungaji, wapanda makanisa, na watenda kazi wa kikristo kwa ajili ya huduma bora na yenye ufanisi katika mazingira ya mijini, ikiwemo Mtaala wa Capstone, ambao ni mtaala wa The Urban Ministry Institute wa ngazi ya seminari wenye moduli kumi na sita uliotengenezwa maalum kwa ajili ya kuwaendeleza viongozi wa makanisa ya mjini.
5
Made with FlippingBook Digital Publishing Software